Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 1:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Mungu ni mushuhuda wangu kwamba ninawapenda sana ninyi wote na moyo wa upendo mukubwa wa Yesu Kristo.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 1:8
24 Iomraidhean Croise  

Nina uhakika kwamba nina mushuhuda wangu mbinguni; mwenye kunitetea yuko kule juu.


Hivyo, nafsi yangu inalilia Moabu kama kinubi, na moyo wangu kwa ajili ya muji wa Kiri-Heresi.


Utuchungulie kutoka mbinguni, ee Mungu, uone, utuangalie kutoka makao yako matakatifu na matukufu. Iko wapi bidii yako kwa ajili yetu na nguvu yako? Hatuoni tena upendo na huruma yako.


Efuraimu ni mwana wangu mupendwa; yeye ni mutoto wangu ninayemupenda sana. Ndiyo maana kila mara ninapomutisha, ninaendelea kumukumbuka. Moyo wangu unamwelekea kwa wema; hakika nitamuhurumia. –Ni ujumbe wa Yawe.


Kutokana na huruma kubwa ya Mungu wetu, atatutumia mwangaza kutoka juu.


Mungu ambaye ninamwabudu kwa roho yangu yote kwa njia ya kutangaza Habari Njema ya Mwana wake, ni mushuhuda wangu kwamba ninawakumbuka siku zote


Ninasema ukweli kwa kuungana na Kristo. Na kwa uongozi wa Roho Mutakatifu zamiri yangu inanihakikishia kwamba sisemi uongo:


Tunafurahi wakati ninyi munapokuwa na nguvu, hata ikiwa sisi ni zaifu. Nasi tunawaombea kusudi mupate kuwa wakamilifu.


Sisi hatukuwafungia mioyo yetu, lakini ni ninyi ndio muliotufungia moyo wenu.


Mapendo yake kwa ajili yenu yanazidi kuongezeka anapokumbuka vile mulivyokuwa tayari kumutii na vile mulivyomupokea kwa woga na kutetemeka.


Ninaapa mbele ya Mungu kuwa sisemi uongo katika maneno haya ninayowaandikia.


Kwa maana ninyi wote mumekuwa wana wa Mungu kwa njia ya imani na kuungana na Yesu Kristo.


Watoto wangu wapendwa, kama vile mwanamuke anavyopata uchungu wa kuzaa, mimi vilevile, ninapata tena uchungu kwa ajili yenu mpaka mutakapokuwa na hali inayokuwa kama ya Kristo ndani yenu.


Maisha yenu katika kuungana kwenu na Kristo si yanawatia ninyi nguvu? Nao upendo wake si unawafariji ninyi? Si munaishi katika ushirika na Roho Mutakatifu? Si muko na moyo mwema na wa huruma?


Yeye yuko na hamu sana kuwaona ninyi wote, naye anahuzunika sana kwa sababu mulisikia kwamba alikuwa mugonjwa.


Kwa hiyo wandugu zangu wapendwa, niko na hamu sana ya kuwaona tena. Ninyi ndio munaokuwa furaha yangu na zawadi ya ushindi nitakayopokea. Ninyi wapendwa wangu, ninawaomba musimame imara katika ushirika wenu na Bwana.


Ninataka mujue jinsi ninavyofanya kazi kwa bidii kwa ajili yenu, kwa ajili ya waamini wa Laodikia na kwa ajili ya wote ambao hawajapata kuniona bado.


Ninyi ni watu wa Mungu, yeye amewapenda na kuwachagua kwa ajili yake mwenyewe. Kwa hiyo, mukuwe na moyo wa huruma, wema, unyenyekevu, upole na uvumilivu.


Kama vile munavyojua, hata siku moja hatukutumia masemi ya kujipendekeza kwa watu wala hatukutamani kupata mali kwa uficho; Mungu ni mushuhuda wetu.


Sisi tunawapenda sana hata tumekuwa tayari, si kuwatolea Habari Njema ya Mungu tu, lakini kutoa maisha yetu kwa ajili yenu vilevile. Ni vile kwa sababu ninyi mumekuwa kweli wapendwa wetu.


Nikikumbuka machozi yako, ninatamani sana kukuona kusudi nipate kujazwa na furaha.


Sasa ninamurudisha kwako, naye ni kama moyo wangu mimi mwenyewe.


Ndiyo, ndugu yangu, ninakusihi unisaidie kwa njia hii kwa ajili ya Bwana, unitulize moyo kama vile ndugu katika Kristo.


Mutu akiwa na mali ya dunia hii naye akimwona ndugu yake katika hitaji, lakini hataki kumusikilia huruma, mutu yule anaweza kusema kwamba anamupenda Mungu?


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan