Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Wafilipi 1:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Ni haki kwangu kuwa na mafikiri haya kwa ajili yenu ninyi wote, kwa sababu ninawakumbuka kila mara. Kwa maana mumeshiriki pamoja nami katika neema ile Mungu aliyonipatia, ingawa sasa niko katika kifungo hata na wakati nilipokuwa huru kutetea na kuimarisha Habari Njema.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Wafilipi 1:7
34 Iomraidhean Croise  

Lakini kitu kimoja ninachojua tu, ni kwamba katika kila muji Roho Mutakatifu ananihakikishia kwamba vifungo na mateso vinaningojea.


Halafu huyo mwongozi akamujongelea Paulo, akamukamata na kuamuru afungwe na minyororo miwili. Kisha akauliza: “Mutu huyu ni nani? Naye amefanya nini?”


Upendo hauchoki na mambo yote, unaamini mambo yote, unatumaini mambo yote na kuvumilia mambo yote.


Ninafanya hayo yote kwa ajili ya Habari Njema kusudi nipate sehemu ya baraka zake.


Ninyi wenyewe ni kama barua yetu ya ushuhuda iliyoandikwa katika mioyo yetu na watu wote wanaweza kuitambua na kuisoma.


Sisemi vile kwa kuwahukumu. Kwa maana, kama vile nilivyokwisha kusema, ninyi ni wapendwa wetu, ikiwa katika kuishi au katika kufa.


Kwa maana kwa wale wanaoungana na Kristo Yesu, kutahiriwa au kutokutahiriwa hakufai kitu. Kitu kinachofaa ni imani inayotenda kazi kwa upendo.


Kufuatana na mambo hayo, mimi Paulo, mufungwa wa Yesu Kristo kwa ajili yenu ninyi watu wa mataifa mengine, ninamwomba Mungu.


Kwa hivi basi, mimi ninayekuwa mufungwa kwa sababu ninamutumikia Bwana, ninawasihi muishi sawa inavyostahili kufuatana na mwito Mungu aliowatolea.


Mimi ni mujumbe wa Habari ile Njema, ijapokuwa sasa ninakuwa katika kifungo. Basi muniombee kusudi nipate kusema kwa uhodari, sawa inavyonipasa kusema.


Wandugu zangu, ninataka mujue kwamba mambo yaliyonifikia yamesaidia kwa kuendelesha Habari Njema.


Kutokana na hayo, walinzi wote wa nyumba ya mufalme pamoja na wengine wote, wanajua kwamba niko katika kifungo kwa sababu ninamutumikia Kristo.


Kwa ajili ya kufungwa kwangu, wandugu wengi wamemwamini Bwana na kuwa na bidii sana ya kutangaza Neno la Mungu pasipo woga.


kwa namna munashirikiana nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema, tangu mwanzo mpaka sasa.


Munajua ninyi wenyewe namna Timoteo alivyojionyesha kwamba anastahili, kwa maana alitumika kazi ya kueleza Habari Njema pamoja nami kama vile mwana anavyotumika na baba yake.


Lakini, mumefanya vizuri kwa kushirikiana pamoja nami katika taabu yangu.


Ninyi Wafilipi munajua vizuri wenyewe kwamba nilipotoka Makedonia, tangu mwanzo wa kuhubiri Habari Njema, ni ninyi tu ndilo kanisa moja lililoshirikiana nami katika mambo ya utoaji na upokeaji.


Na wewe vilevile mutumishi mwenzangu mwaminifu, ninakuomba uwasaidie wanawake hao, kwa maana walisumbuka sana pamoja nami katika kazi ya kutangaza Habari Njema. Kuko vilevile Klementi na wenzangu wengine wa kazi. Hao wote majina yao yameandikwa katika kitabu cha uzima.


Mimi Paulo ninawatumia salamu zangu, nikiziandika kwa mukono wangu mwenyewe. Musisahau kwamba mimi ningali katika kifungo. Ninawatakia neema kutoka kwa Mungu.


Mutuombee sisi vilevile kusudi Mungu atufungulie njia ya kuhubiri neno lake tupate kutangaza ujumbe wa siri juu ya Kristo. Ni kwa ajili ya ujumbe ule mimi niko sasa katika kifungo.


Kwa maana ninyi wote ni watu wanaoishi katika mwangaza, ndio watu wa muchana. Sisi si watu wa usiku wala wa giza.


Basi, usisikie haya ya kutoa ushuhuda kwa ajili ya Bwana wetu, wala usisikie haya kwa sababu yangu mimi ninayekuwa katika kifungo kwa ajili yake. Lakini ushiriki nami katika mateso kwa ajili ya Habari Njema, kufuatana na uwezo unaopewa na Mungu.


Mimi ninateswa na kufungwa sawa mutenda maovu kwa sababu ninahubiri Habari Njema hii. Lakini Neno la Mungu halifungwi.


Ningalipenda Onesimo abakie pamoja nami kwa kunisaidia pahali pako wakati ninapokuwa mufungwa kwa sababu ya Habari Njema.


Kwa sababu hiyo, wandugu zangu, ninyi ambao mumeitwa na Mungu na kuwa watu wake kama vile sisi, mufikiri sana juu ya Yesu, anayekuwa mutume na Kuhani Mukubwa wa imani tunayotangaza.


Lakini mufurahi kwa sababu munashiriki katika mateso ya Kristo. Na kwa hiyo mutashangilia kwa furaha wakati atakapoonekana katika utukufu.


Ninawaonya wazee wa kanisa wanaokuwa kati yenu. Mimi vilevile ni muzee mwenzenu, nami ni mushuhuda wa mateso ya Kristo na zaidi ya hii nitashiriki katika utukufu ule utakaotokea.


Ninaona kwamba ni vema niwaamushe kwa njia ya kuwakumbusha mambo haya wakati wote wa maisha yangu.


Sisi tunajua kwamba tumeponyoka lufu na kupata uzima kwa sababu tunawapenda wandugu zetu. Mutu asiyekuwa na upendo ni kama mufu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan