Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 9:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Siku ya makumi mbili na ine ya mwezi ule wa saba, watu wa Israeli wakakusanyika, wakifunga kula na kuvaa nguo za magunia na kujipakaa udongo juu ya kichwa kwa kuonyesha majuto juu ya zambi zao.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 9:1
22 Iomraidhean Croise  

Siku iliyofuata, mutu mumoja kutoka kambi ya Saulo, nguo zake zikiwa zimepasuka kwa huzuni na akiwa na mavumbi juu ya kichwa, alimwendea Daudi. Alipomufikia Daudi, alijitupa uso mpaka chini mbele yake kwa heshima.


Yosafati akashikwa na woga, akamwomba Yawe amwongoze. Akatangaza kwamba watu wote katika inchi ya Yuda wafunge kula.


Siku iliyofuata ambayo ilikuwa siku ya makumi mbili na tatu ya mwezi wa saba, Solomono akawaaga watu waende kwao, wakishangilia na kufurahi ndani ya moyo kwa sababu ya mazuri ambayo Yawe alimutendea Daudi, Solomono na kwa watu wake Waisraeli.


Kisha, nikatoa maagizo kuwa sisi wote tufike karibu na muto Ahara kusudi tufunge kula chakula na kujinyenyekeza mbele ya Mungu wetu na kumwomba atulinde na kutuongoza katika safari yetu pamoja na watoto wetu.


Kwa hiyo tukafunga na kumwomba Mungu atulinde, naye akayasikia maombi yetu.


Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


“Kwenda uwakusanye pamoja Wayuda wote wanaokuwa katika muji wa Susani. Mufunge, musikule wala musikunywe kwa siku tatu, usiku na muchana, kwa ajili yangu. Na mimi na wajakazi wangu tutafanya vile vile. Kisha, nitamwendea mufalme, ingawa ni kinyume cha sheria. Kama ni kuuawa, niuawe.”


Katika kila jimbo, mara tu amri ya mufalme ilipotangazwa, kilio kikubwa kiliwapata Wayuda. Wakafunga, wakalia na kuomboleza; na wengi wao wakalala katika majivu wakiwa wamevaa magunia.


Walipomwona kwa mbali hawakumutambua. Basi, wakaanza kulalamika na kulia. Wakapasua nguo zao, wakarusha mavumbi katika anga na juu ya vichwa vyao.


Siku hiyo, Yawe wa majeshi alitaka mulie na kuomboleza, munyoe nywele na kuvaa nguo za gunia.


Lakini hata sasa, munirudilie kwa moyo wote, kwa kufunga kula, kwa kulia na kuomboleza. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Uwaambie Waisraeli hivi: Tangu siku ya kumi na tano ya mwezi huo wa saba mutafanya sikukuu ya vibanda kwa muda wa siku saba kwa heshima ya Yawe.


Kisha kuvuna mashamba yenu mutafanya sikukuu kwa muda wa siku saba, tangu siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba. Siku ya kwanza itakuwa siku ya mapumziko na hata siku ya nane.


Yoshua akapasua nguo yake, yeye pamoja na wazee wa Israeli. Wakajitupa chini ya Sanduku la Yawe mpaka magaribi; wakajitia mavumbi juu ya vichwa vyao.


Nami nitawatuma washuhuda wangu wawili, wakiwa wamevaa nguo za kilio. Nao watatangaza ujumbe wa Mungu kwa muda wa siku elfu moja mia mbili na makumi sita.”


Watu wote wa jeshi la Waisraeli wakaenda Beteli. Wakaikaa kule mbele ya Yawe wakiomboleza na kufunga mpaka magaribi. Wakamutolea Yawe sadaka za kuteketezwa kwa moto na sadaka za amani.


Siku hiyohiyo, mutu mumoja wa kabila la Benjamina alikimbia kutoka mustari wa mbele wa mapigano mpaka Shilo nazo nguo zake zikiwa zimechanika na akiwa na mavumbi kwenye kichwa.


Hivyo, Waisraeli wote wakakusanyika kule Misipa. Walichota maji na kuyamimina mbele ya Yawe, wakafunga kula chakula siku ile yote na kusema: “Tumetenda zambi mbele ya Yawe.” Samweli akakuwa mwamuzi wa Waisraeli kule Misipa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan