Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 8:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Watu waliposikia Sheria, wakaguswa ndani ya mioyo yao, halafu wote wakaanza kulia. Hivyo Nehemia aliyekuwa mutawala na Ezra kuhani na mwandishi, pamoja na Walawi waliofundisha watu wakawaambia watu wote: “Siku hii ni siku takatifu kwa Yawe, Mungu wenu, hivyo musiomboleze wala kulia.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 8:9
30 Iomraidhean Croise  

Mufalme aliposikia maneno ya Kitabu cha Sheria, akapasua nguo zake.


Wakati uliposikia niliyosema juu ya pahali hapa na juu ya wakaaji wake, kwamba watakuwa ukiwa na kulaaniwa, ulijuta na kunyenyekea mbele yangu, hata ukapasua nguo yako na kulia mbele yangu. Basi, nami vilevile nimekusikia.


Kwa muda murefu sasa, Waisraeli wameishi bila Mungu wa kweli, wala makuhani wa kuwafundisha, na bila Sheria.


Mufalme Hezekia aliwasifu na kuwatia moyo makuhani kwa sababu waliendesha ibada kwa ujuzi mwingi. Nyuma ya kumaliza siku saba ambamo watu walikula, wakatoa sadaka za amani na kumutukuza Yawe, Mungu wa babu zao,


Mufalme aliposikia maneno ya Sheria akapasua nguo yake.


“Mwende mutafute shauri kutoka kwa Yawe kwa ajili yangu na kwa ajili ya watu ambao wamebaki katika Israeli na Yuda, juu ya maneno yanayokuwa katika kitabu kilichopatikana. Kwa sababu kasirani ya Yawe imetuangukia maana babu zetu hawakushika Neno la Yawe wala kufanya yaliyoandikwa humo.”


Pamoja na hayo, akawapa Walawi waliowafundisha watu wa Israeli na ambao walitakaswa kwa ajili ya Yawe, maagizo haya: “Muweke Sanduku takatifu ndani ya nyumba ambayo Solomono mwana wa Daudi, mufalme wa Israeli aliyojenga; hamuhitaji kulibebabeba tena juu ya mabega. Sasa mumutumikie Yawe, Mungu wenu, na watu wake Waisraeli.


Mutawala akawaambia kwamba hawaruhusiwi kushiriki chakula kitakatifu sana, mpaka kukuwe kuhani atakayeweza kutoa shauri kwa njia Urimu na Tumimu.


Huu ndio mufano wa barua ambayo Artasasta alimupa Ezra, kuhani na mwandishi, na mwenye ujuzi katika amri na masharti ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Kutokana na haya yote yaliyotokea, sisi tunaweka agano imara kwa maandiko na wakubwa wetu, Walawi na makuhani wanatia sahihi zao na muhuri wao.


Watu hao waliishi wakati wa Yoyakimu mwana wa Yesua mujukuu wa Yosadaki na vilevile wakati wa Nehemia aliyekuwa liwali wa jimbo; na hata wakati wa Ezra kuhani na mwandishi.


Mutawala akawaambia kwamba hawaruhusiwi kushiriki kwa chakula kitakatifu sana, mpaka kuhani anayeweza kutumia Urimu na Tumimu afike.


Wakubwa wa ukoo walitoa kilo mia moja makumi sita na nane za zahabu, na kilo elfu moja mia mbili na makumi tano za feza.


Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.


wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,


na kuwapa wale wanaoomboleza katika Sayuni taji la maua pahali pa majivu juu ya kichwa, mafuta ya kuangarisha kwa furaha pahali pa maombolezo, nguo ya sifa pahali pa moyo muzito. Nao wataitwa miti ya mialo ya haki, Yawe aliyopanda kuonyesha utukufu wake.


Watu wangu wameangamia kwa kutonijua, maana wewe kuhani umekataa mafundisho. Nimekukataa kuwa kuhani wangu. Kwa maana umeisahau sheria ya Mungu wako, nami vilevile nitawasahau watoto wako.


Uwaambie watu wa Israeli hivi: Siku ya kwanza ya mwezi wa saba mutafanya siku ya mapumziko, siku ya ukumbusho itakayotangazwa kwa mulio wa baragumu na kufanya mukutano mutakatifu.


Zaidi ya hayo yote, munaifunika mazabahu ya Yawe kwa machozi yenu, mukilia na kuomboleza kwa sababu yeye hazikubali tena sadaka munazomutolea.


Kwa sababu hakuna mutu atakayehesabiwa haki mbele ya Mungu kwa kuwa anatii Sheria, maana Sheria inamusaidia mutu tu kwa kutambua kwamba amefanya zambi.


Zamani nilikuwa muzima pasipo kujua Sheria, lakini wakati amri ilipotokea, zambi ikaanza kutenda kazi,


Huko mutafurahi mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na watoto wenu wanaume na wanawake, watumishi na wajakazi wenu, na Walawi wanaoishi kati yenu kwa sababu hawana sehemu wala urizi kati yenu.


Huko, mutakula mbele ya Yawe, Mungu wenu, na mutafurahi ninyi pamoja na watu wa nyumba zenu kwa ajili ya mafanikio yenu Yawe, Mungu wenu, aliyowabarikia.


Mutafurahia mbele ya Yawe, Mungu wenu, ninyi pamoja na wana wenu na wabinti zenu, watumishi wenu, Walawi, wageni, wayatima na wajane ambao wanaishi pamoja nanyi. Mufanye haya katika pahali Yawe, Mungu wenu, atakapochagua kwa ajili ya jina lake.


Sikukula sehemu ya kumi yoyote nilipokuwa ninaomboleza; sikuitoa inje ya nyumba yangu nilipokuwa muchafu na sikutoa sehemu ya kumi hiyo kwa wafu. Nimekutii ee Yawe, Mungu wangu; nimefanya kila kitu ulichoamuru juu ya sehemu ya kumi.


Musikitike, mulie na kulalamika. Kucheka kwenu kugeuke kuwa kilio, na furaha yenu igeuke kuwa huzuni.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan