Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 8:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Kisha Ezra akawasomea watu wote wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa Sheria ya Musa akiwa mbele ya Mulango wa Maji tangu asubui mpaka saa sita za muchana. Watu wote wakatega masikio yao na kusikiliza kwa uangalifu kitabu cha Sheria.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 8:3
25 Iomraidhean Croise  

Sisi wote, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango, waimbaji, watumishi wa hekalu na watu wote waliojitenga na mataifa jirani kufuata sheria ya Mungu pamoja na wake zao, wana wao, na wabinti zao, wote wenye maarifa na ufahamu,


Katika siku ile ya sherehe, kitabu cha Musa kikasomwa na ikajulikana kwamba Waamoni na Wamoabu hawaruhusiwi kuingia katika mukutano wa watu wa Mungu.


Kisha watu wote, kwa nia moja, wakakusanyika katika Yerusalema kwenye kiwanja kinachokuwa karibu na Mulango wa Maji. Wakamwambia Ezra, mwandishi, alete kitabu cha sheria ya Musa ambayo Yawe aliwapa watu wa Israeli.


Kila siku, tangu siku ya kwanza mpaka ya mwisho, Ezra aliwasomea watu kitabu cha Sheria ya Mungu. Wakafanya sikukuu ile kwa muda wa siku saba. Na siku ya nane wakafanya mukutano mukubwa wa kufunga sikukuu, kama vile ilivyoagizwa.


Ezra, mwandishi, alikuwa akisimama kwenye mimbari ya mbao iliyotengenezwa kwa kusudi lile; na kwenye mukono wake wa kuume watu hawa walikuwa wakisimama: Matitia, Sema, Anaya, Uria, Hilkia na Masea; na kwenye mukono wake wa kushoto kulikuwa kunasimama watu hawa: Pedaya, Misaeli, Malkiya, Hasumu, Hasubadana, Zakaria na Mesulamu.


Ezra akasimama kwenye mimbari mbele ya watu wote, nao wakakuwa wanamukazia macho yao kwa utulivu mukubwa. Mara tu Ezra alipokifungua kitabu cha Sheria, watu wote wakasimama wima.


Daudi mwenyewe anamwita Kristo ‘Bwana’; namna gani basi Kristo anaweza kuwa Mwana wake?” Kundi kubwa la watu walimusikiliza Yesu kwa furaha.


Lakini hawakupata namna ya kumwua, kwa sababu watu wote walimusikiliza kwa uangalifu.


“Basi mufanye angalisho na jinsi munavyosikia maneno. Kwa maana mutu anayekuwa na kitu, ataongezewa kingine, lakini mutu asiyekuwa na kitu, atanyanganywa kile anachozania kuwa nacho.”


Na nyuma ya kusoma katika vitabu vya Sheria na vya manabii, wakubwa wa ile nyumba ya kuabudia wakatuma mutu kwa kuwaambia: “Wandugu, ikiwa muko na maneno ya kuwatia watu moyo, muyaseme.”


Wakaaji wa Yerusalema na wakubwa wao hawakumutambua Yesu wala maandiko ya manabii yaliyosomwa kila siku ya Sabato. Lakini ingawa hivi wakatimiza maandiko yale kwa njia ya kumuhukumu kufa.


Kwa maana tangu zamani Sheria ya Musa inasomwa kila siku ya Sabato katika nyumba za kuabudia na kuhubiriwa katika kila muji.”


Na kati ya wanawake wale kulikuwa mwanamuke mumoja aliyeitwa Ludia, wa muji Tuatera. Yeye alikuwa muchuuzi wa nguo nyekundu za bei kali na mwenye kuogopa Mungu. Mwanamuke yule akatusikiliza kwa maana Bwana alimufungua moyo kusudi apate kufuata kabisa maneno Paulo aliyosema.


Watu hao walikuwa wenye nia nzuri zaidi kuliko watu wa Tesalonika; nao walipokea Neno la Mungu kwa hamu kubwa. Kila siku walichunguza Maandiko Matakatifu wapate kujua kwamba maneno Paulo aliyosema yalikuwa ya haki.


Kisha Paulo akapanda juu tena kwenye gorofi, akamega mukate na kuukula. Akaendelea kuhubiri kwa muda murefu mpaka saa za mapambazuko, na kisha akaondoka.


Siku ya kwanza ya juma, tulikuwa tunakusanyika kwa kumega mukate. Paulo akasemezana na watu na kuendelea kuwahubiria mpaka katikati ya usiku, kwa sababu alikusudia kuondoka kesho yake.


Halafu wakapanga siku ya kukutana na Paulo. Na siku ile watu wengi zaidi wakamufikia pahali alipopanga. Na tangu asubui mpaka magaribi Paulo akawaelezea mambo mengi na kutoa ushuhuda juu ya habari za Ufalme wa Mungu. Alitaka wasadiki habari za Yesu akitaja maneno ya Sheria ya Musa na ya vitabu vya manabii.


Basi, Musa akaandika sheria hiyo, akawapa makuhani wa ukoo wa Lawi ambao walikuwa wakibeba Sanduku la Agano la Yawe, na wazee wote wa Israeli.


Inatupasa tena kumushukuru Mungu siku zote kwa ajili ya jambo hili: muliposikia neno la Mungu kutoka kwetu, hamukulikubali kama vile neno la mutu, lakini kama vile kweli ndilo neno la Mungu. Na neno lile ndilo linalofanya kazi ndani ya mioyo yenu ninyi wanaoamini.


Hakuna neno lililoamriwa na Musa ambalo Yoshua hakulisoma mbele ya Waisraeli, kati yao kukiwa wanawake, watoto na wageni.


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa!


“Mwenye kuwa na masikio, asikie vizuri vile Roho anavyoyaambia makanisa.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan