Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 7:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

6 Wale waliokuwa katika uhamisho kule Babeli, walirudi Yerusalema na katika inchi ya Yuda, kila mumoja akarudi katika muji wake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babeli tangu mufalme Nebukadneza alipowahamishia kule wakiwa watumwa.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 7:6
10 Iomraidhean Croise  

Nebuzaradani, mukubwa wa waaskari wa mufalme, akawapeleka katika uhamisho watu waliokuwa wamebakia katika muji na wale wote waliokuwa wamejitoa wenyewe kwa mufalme wa Babeli pamoja na watu wengine wote.


Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.


Lakini kitabu kikapatikana katika muji wa Akimeta katika jimbo la Media, nacho kilikuwa na maagizo haya:


Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”


Waliporudi waliongozwa na Zerubabeli, Yesua, Nehemia, Azaria, Ramia, Nahamani, Mordekayi, Bilsani, Misipereti, Bigwayi, Nehumu na Bana. Hii ndiyo jumla ya watu wa ukoo za Waisraeli waliorudi toka katika uhamisho:


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan