Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 7:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nyuma ya ukuta kumalizika, milango yote kuwa tayari, na kuchaguliwa kwa walinzi wa milango, waimbaji na Walawi,

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 7:1
12 Iomraidhean Croise  

Hivyo, wakaondoka katika kambi ya Waaramu na kuwaita walinda milango ya muji na kuwaambia: “Tulikwenda katika kambi ya Waaramu na hatukuweza kumwona wala kumusikia mutu yeyote. Farasi na punda wangali wanafungwa, na mahema yako kama walivyoyaacha.”


Mufalme Hezekia akawapanga tena makuhani na Walawi katika makundi, akamupa kila mumoja wao kazi kufuatana na utumishi wake katika sehemu mbalimbali za hekalu la Yawe. Kazi ile ni pamoja na utoaji wa sadaka za kuteketeza kwa moto na za amani, za shukrani na za kusifu.


Basi, watu wakaanza kazi katika mwezi wa pili wa mwaka wa pili nyuma ya kufikia kwenye nyumba ya Mungu katika Yerusalema. Zerubabeli, mwana wa Saltieli, Yesua mwana wa Yosadaki, wandugu zao wengine, makuhani, Walawi na watu wengine wote waliorudi Yerusalema kutoka katika uhamisho, wakajiunga nao katika kazi hiyo. Walawi wote waliokuwa na umri wa miaka makumi mbili au zaidi, walichaguliwa kwa kusimamia kazi ya kuijenga upya nyumba ya Yawe.


Kuhani, wa uzao wa Haruni atakuwa pamoja na Walawi wanapokea zaka. Halafu Walawi watapeleka sehemu moja ya kumi ya zaka zote zilizotolewa katika nyumba ya Mungu kwenye vyumba na gala.


Na katika miji mingine, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango na wazao wa watumishi wa Solomono, walikaa katika maeneo yao wenyewe, katika miji yao.


Viongozi wa Walawi Hasabia, Serebia, Yesua mwana wa Kadimieli walisimama kuelekeana na wandugu zao walipangwa kwa kuimba nyimbo za kusifu na kushukuru, kufuatana na amri ya mufalme Daudi, mutu wa Mungu.


Kisha Sanibalati, Tobia, Gesemi, Mwarabu na waadui zetu wengine, waliposikia kwamba tumemaliza ujenzi wa ukuta na kwamba hakuna pahali penye kubomoka (ingawa tulikuwa bado hatujaweka milango),


Basi, ukuta ikamalizika siku ya makumi mbili na tano ya mwezi wa Eluli; nayo ilidumu muda wa siku makumi tano na mbili.


Vilevile wakanielezea matendo mema ya Tobia, na wakakuwa wanamupelekea habari zangu. Naye akakuwa ananiandikia barua kwa kunitisha.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan