Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 5:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Kisha nikawaambia: “Jambo munalofanya si zuri. Haiwapasi kumwogopa Mungu wetu kwa kuzuia mataifa mengine yanayokuwa waadui zetu yasituzarau?

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 5:9
21 Iomraidhean Croise  

Abrahamu akamujibu: “Nilifanya hivyo kwa sababu hakuna anayemwogopa Mungu pahali hapa na kwamba mungeniua kusudi mumutwae muke wangu.


Siku ya tatu Yosefu akawaambia: “Kwa sababu ninamwogopa Mungu, mufanye hivi kusudi mupate kuishi:


Hata hivyo, kwa sababu kwa tendo lako umemuzarau kabisa Yawe, mutoto wako atakufa.”


Watu wa Yuda wakakuwa wanalalamika wakisema: “Tunachoka na kubeba mizigo na bado kuna takataka nyingi za kubeba. Hatuwezi kuendelea kujenga ukuta.”


Zaidi ya hayo, mimi mwenyewe, wandugu zangu na watumishi wangu tumewakopesha wandugu zetu feza na ngano. Na hatutadai faida yoyote.


Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.


Nani anayetambua uzito wa hasira yako? Nani anayeona matokeo ya kasirani yako?


Mutesaji mukali anamushawishi jirani yake na kumwongoza katika njia mbaya.


Si vizuri kumwazibu mutu asiyekuwa na kosa; ni kosa kuwapiga fimbo wenye heshima.


Si vizuri kumupendelea mutu mwovu, na kumunyima sheria mutu wa haki.


Haifai mutu kuwa bila akili; mwenda harakaharaka anajikwaa.


Hii ni misemo mingine ya wenye hekima. Kupendelea watu katika hukumu si vizuri.


Hata walipokuwa kati ya mataifa walilikufuru jina langu takatifu, hata watu wakasema hivi juu yao: Hawa ndio wale watu wa Yawe, lakini wamelazimishwa kuondoka katika inchi yake!


Usimwombe akulipe faida ya namna yoyote. Lakini umwogope Mungu, naye ndugu yako apate kuishi pamoja nawe.


Wakati ule, kanisa lilikuwa na amani katika Yudea yote, Galilaya na Samaria. Vilevile lilizidi kupata nguvu na kuendelea kumwogopa Bwana, nalo liliongezeka kwa musaada wa Roho Mutakatifu.


Kwa maana kama ilivyoandikwa katika Maandiko Matakatifu: “Kwa sababu yenu, jina la Mungu linatukaniwa katikati ya watu wa mataifa mengine.”


Kwa sababu hiyo, ninataka wajane wanaokuwa wangali vijana waolewe, wazae watoto na kutunza nyumba zao, kusudi waadui wasipate nafasi ya kutuchongea.


na kuwa wenye utaratibu, wenye maisha safi, wenye kutunza nyumba zao vizuri, wema na wenye kutii waume wao, kusudi Neno la Mungu lisitukaniwe.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Musifanye hivyo wana wangu, kwa sababu mambo hayo ninayoyasikia kutoka kwa watu wa Yawe ni mabaya.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan