Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 5:15 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

15 Watawala walionitangulia walikuwa muzigo muzito kwa watu wakiwadai chakula na divai. Zaidi ya hiyo waliwalipisha vikoroti makumi ine vya feza. Hata watumishi wao waliwatesa watu. Lakini, mimi sikufanya hivyo, maana nilimwogopa Mungu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 5:15
19 Iomraidhean Croise  

Abrahamu akamujibu: “Nilifanya hivyo kwa sababu hakuna anayemwogopa Mungu pahali hapa na kwamba mungeniua kusudi mumutwae muke wangu.


Siku ya tatu Yosefu akawaambia: “Kwa sababu ninamwogopa Mungu, mufanye hivi kusudi mupate kuishi:


Nilikuwa na juhudi nyingi katika ujenzi mupya wa ukuta huu na sikujipatia hata shamba. Hata watumishi wangu wote walifanya kazi hii kwa bidii.


Kisha nikawaambia: “Jambo munalofanya si zuri. Haiwapasi kumwogopa Mungu wetu kwa kuzuia mataifa mengine yanayokuwa waadui zetu yasituzarau?


Maana hasara kutoka kwa Mungu ni kitisho kwangu; mimi siwezi kusimama mbele ya ukubwa wake.


Haleluia! Heri mutu anayemuheshimu Yawe, anayefurahia sana kushika amri zake.


lakini anapendezwa na watu wanaomuheshimu, ndio wanaotegemea wema wake.


Kwa wema na uaminifu mutu anaondoa uovu. Kwa kumwogopa Yawe anaepuka ubaya.


Mutawala akisikiliza mambo ya uongo, wakubwa wake wote watakuwa waovu.


Nani kati yenu anayemwogopa Yawe? Nani anayetii maneno ya mutumishi wake? Kama kuna mutu anayetembea katika giza bila taa, amutumainie Yawe, na kumutegemea Mungu wake.


Nikalinunua shamba hilo linalokuwa kule Anatoti, kutoka kwa binamu yangu Hanameli, nikamulipa bei yake vikoroti kumi na saba vya feza.


Watumwa wanatutawala, wala hakuna wa kutuokoa toka katika mikono yao.


Na kama mukiwasalimia wandugu zenu tu, munatenda tendo gani la kupita wengine? Hata wapagani wanatendeana vile!


Wakati nilipokuwa kwenu, sikumulemea mutu yeyote nilipohitaji kitu fulani, kwa maana wandugu waliotoka Makedonia waliniletea vitu vyote nilivyohitaji. Nilijiangalia vizuri katika mambo yote kusudi nisiwalemee, nami nitaendelea kujiangalia vema.


Mumepungukiwa na nini kuliko makanisa mengine, isipokuwa tu kwamba mimi sikuwalemea kwa kupata musaada toka kwenu? Munisamehe kwa kosa hili.


Atatwaa sehemu ya kumi ya ngano zenu na ya zabibu zenu na kuwapa wakubwa wake na watumishi wake.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan