Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 4:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Hivyo, kwenye sehemu za chini za ukuta ambazo zilikuwa bado kumalizika, nyuma ya ukuta, katika pahali pa wazi, nikawapanga watu kulingana na jamaa zao wakiwa na mapanga, mikuki na pinde.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 4:7
29 Iomraidhean Croise  

Nitaweka uadui kati yako na yule mwanamuke, kati ya uzao wako na uzao wake. Yeye ataponda kichwa chako, nawe utamwuma kisigino chake.”


Basi, Yawe akamupelekea makundi ya Wababeli, Waaramu, Wamoabu na Waamoni washambulie inchi ya Yuda na kuiharibu, kulingana na neno la Yawe alilolisema kwa njia ya watumishi wake manabii.


Nyuma ya mambo hayo, majeshi ya Wamoabu na Waamoni pamoja na sehemu ya Wameuni wakashambulia inchi ya Yuda.


Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.


Lakini Sanibalati wa muji wa Muhori na Tobia, Mwamoni, mutumishi wake, waliposikia kwamba nimekuja kwa kushugulikia hali njema ya watu wa Israeli, hawakufurahia kabisa jambo hilo.


Lakini Sanibalati, Muhori, Tobia, Mwamoni mutumishi wake, na Gesemi, Mwarabu, waliposikia hayo, wakatucheka na kutuzomea wakisema: “Ni kitu gani hiki munachotenda? Munataka kumwasi mufalme?”


Lakini Sanibalati, Tobia, Waarabu, Waamoni na Waasidodi waliposikia kwamba ujenzi mupya wa ukuta wa Yerusalema ulikuwa unasonga mbele na kwamba nafasi zilizobomoka katika ukuta zimezibwa, wao walizidi kukasirika.


Wayuda waliokaa kati ya waadui zetu waliposikia maneno yao, mara kwa mara, walitufikia mara kumi wakisema: “Watakuja toka kila pahali wanapokaa na kutushambulia.”


Nilipoona kwamba watu walikuwa na hofu nikawaambia wakubwa, wasimamizi na watu wote kwa jumla: “Musiwaogope hata kidogo. Mukumbuke Bwana anayekuwa mukubwa na wa kutisha, basi mupigane kwa ajili ya wandugu zenu, wana wenu, wabinti zenu, wake zenu na nyumba zenu.”


Waadui zetu katika mataifa jirani, waliposikia kwamba kazi tumeimaliza, wakaogopa na kupata haya sana; maana walijua hakika kwamba kazi hii ilikamilika kwa musaada wa Mungu wetu.


wageni wote walioishi katika inchi ya Misri; wafalme wote wa inchi ya Uzi; wafalme wote wa miji ya Wafilistini, Askeloni, Gaza, Ekuroni na mabaki ya Asidodi;


Kisha, Isimaeli aliwakamata wabinti wa mufalme mateka na watu wote waliobaki kule Misipa, watu ambao Nebuzaradani, mukubwa wa walinzi, alikuwa amewaweka chini ya ulinzi wa Gedalia mwana wa Ahikamu. Isimaeli mwana wa Netania, aliwakamata mateka hao, akaondoka, akaenda kwa Waamoni.


Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.


Nitaondoa wakaaji wa muji wa Asidodi, pamoja na mutawala wa Asikeloni. Nitanyoosha mukono wangu kwa kuazibu muji wa Ekuroni, na Wafilistini wote waliobaki wataangamia. Ni mimi Yawe ninayesema hivyo.


Mutangaze katika nyumba nzuri kule Asidodi, na katika nyumba nzuri za inchi ya Misri: Mukusanyike kwenye milima inayoizunguka inchi ya Samaria, mujionee fujo kubwa na mateso yanayofanyika kule.


Wajumbe wa lile Baraza Kubwa waliposikia maneno hayo, wakakasirika sana na kutaka kuwaua mitume.


Yule nyoka akamukasirikia yule mwanamuke na kwenda kufanya vita na wazao wake wengine; ndio wale wanaoshika amri za Mungu na kufuata ukweli ulioshuhudiwa na Yesu Kristo.


Lakini akawaambia: “Nitafanya mapatano nanyi kwa shurti hii moja: nitamwongoa kila mumoja wenu jicho lake la kuume. Hivyo nitawapatisha Waisraeli wote haya.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan