Nehemia 4:6 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
6 Wayuda waliokaa kati ya waadui zetu waliposikia maneno yao, mara kwa mara, walitufikia mara kumi wakisema: “Watakuja toka kila pahali wanapokaa na kutushambulia.”
“Lakini, mimi ni nani, na watu wangu ni nani, hata tuweze kutoa kwa mapenzi yetu hivi? Kwa maana vitu vyote vinatoka kwako, tumekutolea vitu vinavyokuwa vyako wewe mwenyewe.
Tena zaidi ya vyote nilivyotoa kwa ajili ya nyumba takatifu, nina hazina yangu ya pekee ya zahabu na feza, na kwa sababu ninapenda nyumba ya Mungu wangu ninaitoa kwa nyumba ya Mungu wangu;
Hivyo, kwenye sehemu za chini za ukuta ambazo zilikuwa bado kumalizika, nyuma ya ukuta, katika pahali pa wazi, nikawapanga watu kulingana na jamaa zao wakiwa na mapanga, mikuki na pinde.
Basi, Yawe akamutia moyo mutawala Zerubabeli wa Yuda pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho. Wakaanza kazi hiyo ya kuijenga upya nyumba ya Yawe wa majeshi, Mungu wao,
awakamilishe katika kila tendo jema kusudi mupate kutimiza mapenzi yake; yeye atimize ndani yetu yale yanayomupendeza, kwa njia ya Yesu Kristo. Yesu atukuzwe milele na milele. Amina.