Wakati ule, Daudi aliambiwa kwamba hata Ahitofeli alikuwa mumoja wa waasi waliojiunga na Abusaloma. Lakini Daudi akaomba akisema: “Ee Yawe, ninakuomba uyafanye mashauri ya Ahitofeli yasifanikiwe.”
Abusaloma pamoja na watu wote wa Israeli wakasema: “Shauri la Husayi ni bora kuliko shauri la Ahitofeli.” Wakakataa shauri la Ahitofeli kwa sababu Yawe alikuwa amepanga kulishinda shauri jema la Ahitofeli kusudi aweze kumuletea Abusaloma hasara.
Wakati ule nikawaambia watu: “Kila mwanaume na mutumishi wake atakaa katika Yerusalema usiku, kusudi tukuwe na ulinzi usiku, na wakati wa muchana wataendelea na kazi.”
Itakuwa kama vile mutu anayefunga safari. Alipotoka kwake akawaachia watumishi madaraka yake, akimupa kila mutu kazi yake. Vilevile akamwagiza mulinzi wa mulango akeshe.
Mufanye bidii sana mupate kuishi katika amani. Mushugulike na mambo yenu ninyi wenyewe na kufanya kazi kwa mikono yenu wenyewe sawa vile tulivyokwisha kuwaagiza.