Nyuma ya hayo, Manase akajenga ukuta mwingine upande wa inje wa muji wa Daudi, upande wa magaribi wa Gihoni, katika bonde, akauendelesha mpaka kwenye Mulango wa Samaki, akauzungusha Ofeli; akauinua juu sana. Pamoja na hayo, akaweka majemadari wa majeshi katika miji yote ya inchi ya Yuda yenye kuta.
Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.
Vilevile ninakuomba kwamba barua ingine iandikwe kwa Asafu mulinzi wa pori la kifalme kusudi anipatie mbao za kutengeneza miimo ya milango ya munara wa hekalu, ukuta wa muji na nyumba yangu nitakamokaa.” Mufalme akakubali ombi langu kwa kuwa Mungu, kwa wema wake, alikuwa pamoja nami.
Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Meremoti mwana wa Uria, mujukuu wa Hakosi. Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Mesulamu mwana wa Berekia, mujukuu wa Mesezabeli. Sehemu inayofuata ikajengwa upya na Zadoki mwana wa Bana.
Kisha Sanibalati, Tobia, Gesemi, Mwarabu na waadui zetu wengine, waliposikia kwamba tumemaliza ujenzi wa ukuta na kwamba hakuna pahali penye kubomoka (ingawa tulikuwa bado hatujaweka milango),