Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 3:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Basi Eliasubu, Kuhani Mukubwa, pamoja na wandugu zake waliokuwa makuhani wakasimama na kuanza kujenga Mulango wa kondoo. Wakautakasa na kutia milango yake; wakaitakasa tangia kwenye Munara wa Mia Moja mpaka Munara wa Hananeli.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 3:1
19 Iomraidhean Croise  

Yesua alizaa Yoyakimu, Yoyakimu alizaa Eliasibu, Eliasibu alizaa Yoyada, Yoyada alizaa Yonatani, Yonatani alizaa Yadua.


Makuhani na Walawi wakajitakasa, vilevile wakatakasa watu, milango na ukuta.


Na kutoka pale, tukapitia kwenye Mulango wa Efuraimu, Mulango wa Yesana, Mulango wa Samaki, Munara wa Hananeli, Munara wa Mia moja mpaka kwenye Mulango wa Kondoo. Tulimalizia maandamano yetu kwenye Mulango wa Walinzi.


Mumoja kati ya wana wa Yoyada mwana wa Kuhani Mukubwa Eliasibu, alioa binti wa Sanibalati kutoka muji wa Beti-Horoni, kwa sababu hiyo nikamufukuza kutoka mbele yangu.


Mbele ya siku ya sherehe, kuhani Eliasibu aliyekuwa amechaguliwa kwa kulinda vyumba vya nyumba ya Mungu wetu, na mwenye ushirika mwema na Tobia,


Sehemu inayofuata tangia kwenye pembe mpaka kwenye mulango wa Eliasibu, Kuhani Mukubwa, ikajengwa upya na Baruku mwana wa Zabayi.


Sehemu inayofuata tangia kwenye mulango wa nyumba ya Eliasibu, Kuhani Mukubwa, mpaka mwisho wa nyumba hiyo, ikajengwa upya na Meremoti mwana wa Uria, mujukuu wa Hakosi.


Sehemu ya mwisho kutokea kwa chumba kwenye pembe mpaka kwenye Mulango wa Kondoo ikajengwa upya na wafua zahabu na wachuuzi.


Kisha Sanibalati, Tobia, Gesemi, Mwarabu na waadui zetu wengine, waliposikia kwamba tumemaliza ujenzi wa ukuta na kwamba hakuna pahali penye kubomoka (ingawa tulikuwa bado hatujaweka milango),


Nyuma ya ukuta kumalizika, milango yote kuwa tayari, na kuchaguliwa kwa walinzi wa milango, waimbaji na Walawi,


Mashairi yanayoelekea muzinduo wa hekalu. Zaburi ya Daudi.


Watu wa Sayuni wafurahi! Watu wa Yuda washangilie, kwa sababu ya hukumu yako ya haki!


Umutambue Mungu katika kila kitu unachofanya, naye atasawanisha njia zako.


Umuheshimu Yawe kwa mali yako, na kwa malimbuko ya mazao yako yote.


Siku zinakuja ambapo muji huu wa Yerusalema utajengwa upya kwa ajili ya Yawe, kutokea kwenye munara wa Hananeli mpaka kwenye mulango wa Pembe.


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Inchi yote, tangu Geba mpaka Rimoni, upande wa kusini wa Yerusalema, itageuzwa kuwa mbuga yenye kunyooka kabisa. Lakini Yerusalema utabaki juu pahali pake tokea mulango wa Benjamina mpaka kwenye mulango wa zamani, hata kwenye mulango wa Konani, tangu munara wa Hanameli mpaka kwenye kikamulio cha mufalme.


Kule Yerusalema, karibu na mulango wa muji huu unaoitwa “Mulango wa Kondoo,” kuna kisima chenye viingilio vitano vyenye paa. Kisima kile kinaitwa katika Kiebrania “Betesaida.”


“Kisha wakubwa watawaambia watu: ‘Kuna mutu yeyote hapa aliyejenga nyumba mupya lakini hajaizindua? Arudie kwake, kusudi asikufie kwenye vita na mutu mwingine aizindue.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan