Nehemia 2:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
3 Nikamujibu: “Ee mufalme, uishi milele! Kwa nini nisikuwe mwenye huzuni wakati Yerusalema ambamo makaburi ya babu zangu uko tupu na milango yake imeteketezwa kwa moto?”
Katika siku ya saba ya mwezi wa tano wa mwaka wa kumi na tisa wa utawala wa Nebukadneza mufalme wa Babeli, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari walinzi wa mufalme, akaingia Yerusalema.
Yoramu alianza kutawala akiwa na umri wa miaka makumi tatu na miwili; akatawala kule Yerusalema kwa muda wa miaka minane. Wakati alipokufa, hakuna mutu yeyote aliyemusikitikia. Alizikwa katika muji wa Daudi, lakini si katika makaburi ya wafalme.
Mufalme Ahazi alikufa na kuzikwa katika muji wa Yerusalema, lakini si katika makaburi ya wafalme wa Israeli. Na Hezekia mwana wake, akatawala pahali pake.
Hezekia akakufa na kuzikwa kwenye sehemu ya juu ya makaburi ya wafalme. Watu wote wa inchi ya Yuda na wakaaji wa Yerusalema wakamutolea heshima kubwa wakati wa kifo chake, naye Manase, mwana wake, akatawala pahali pake.
Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”
Nikatoka nikipitia kwenye Mulango wa Bonde katika njia inayoelekea kwenye Kisima cha Joka na mulango wa Yalala; nikachunguza kuta za muji wa Yerusalema ambazo zilikuwa zimebomolewa pamoja na milango yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto.
Katika siku ya kumi ya mwezi wa tano, mwaka wa kumi na kenda wa utawala wa Nebukadneza, mufalme wa Babeli, Nebuzaradani mukubwa wa waaskari wa mufalme ambaye alimutumikia mufalme wa Babeli, aliingia Yerusalema.
Milango yake imezama ndani ya udongo, ameharibu na kuvunjavunja vifungio vyake. Mufalme na wakubwa wake wako katika uhamisho kati ya mataifa. Hakuna sheria tena, manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Yawe.
Kutokana na kelele za mufalme na wakubwa wake, mama ya mufalme aliingia ndani ya chumba cha karamu, akasema: Uishi milele, ee mufalme! Si lazima mawazo yako yakufazaishe na rangi yako kubadilika.
Alipofika karibu akamwita Danieli kwa sauti ya huzuni: Danieli, mutumishi wa Mungu Mwenye Uzima, Mungu wako unayemutumikia siku zote ameweza kukuokoa na simba hawa?
Halafu wakapatana hivi: Hatutapata kisingizio chochote cha kumushitaki Danieli isipokuwa kama kisingizio hicho kitakuwa kinaelekea Sheria ya Mungu wake.