Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 2:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Katika mwezi wa Nisani, kwa mwaka wa makumi mbili wa utawala wa mufalme Artasasta, wakati divai ilipokuwa mbele yake, nilitwaa divai na kumupatia mufalme. Mpaka sasa nilikuwa sijapata kuwa na huzuni mbele yake.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 2:1
9 Iomraidhean Croise  

Katika mikono yangu nilikuwa na kikombe cha mufalme, basi, nikatwaa zabibu, nikazikamua katika kikombe kile, nikamupa mufalme.”


Kisha akamurudishia mutunza vinywaji cheo chake, apate kumupatia kikombe.


Tena wakati wa utawala wa Artasasta, mufalme wa Persia, Bisilamu, Mitiredati, Tabeli na warafiki zao, wakamwandikia barua mufalme Artasasta. Barua hiyo iliandikwa katika herufi za Kiaramea na kutafsiriwa.


Nyuma ya mambo yale, wakati wa utawala wa mufalme Artasasta wa Persia, kulikuwa mutu mumoja aliyeitwa Ezra. Ezra alikuwa mwana wa Seraya mwana wa Azaria mwana wa Hilkia


Katika mwaka wa saba wa utawala wa mufalme Artasasta, Ezra akafunga safari kutoka Babeli kwenda Yerusalema. Alikwenda pamoja na watu wamoja wa Israeli, makuhani, Walawi, waimbaji, walinzi wa milango na watumishi wa hekalu.


Hili ni simulizi la Nehemia mwana wa Hakalia. Ilitukia kwamba, nilipokuwa katika muji mukubwa wa Susani, katika mwezi wa Kisileu wa mwaka wa makumi mbili,


Ee Bwana, usikilize maombi yangu mimi mutumishi wako na ya watumishi wako wanaofurahia kukutii wewe. Ninakuomba unifanikishe leo, mimi mutumishi wako, na kunijalia kuhurumiwa na mufalme.” Mimi nilikuwa na madaraka ya kumupa mufalme kinywaji.


Katika mwaka wa kumi na mbili wa utawala wa mufalme Ahasuero, katika mwezi wa kwanza unaoitwa Nisani, wakapiga Purimu, maana yake kura, mbele ya Hamani kusudi ajue mwezi na siku ya kuwaangamiza. Basi kura ikaangukia mwezi wa kumi na mbili unaoitwa Adari.


Basi, ujue na kufahamu jambo hili: tangu wakati amri itakapotolewa ya kujengwa upya Yerusalema mpaka kuja kwa yule aliyepakwa mafuta, yule anayekuwa mukubwa, ni muda wa majuma saba. Kwa muda wa majuma makumi saba na mawili, Yerusalema utajengwa upya, wenye barabara kubwa na kuta, lakini wakati huo utakuwa wa taabu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan