Nikamwomba Mungu nikisema: “Ee Mungu, kumbuka mambo yote Tobia na Sanibalati waliyotenda, hata yule Noadia, nabii mwanamuke, na manabii wengine waliotaka kuniogopesha.”
Utamutambua kuhani kuwa aliyetakaswa, maana yeye ndiye anayetolea sadaka ya mukate wa Mungu wako. Utamutambua kuwa mutakatifu, maana mimi Yawe ninayekutakasa wewe ni mutakatifu.
Kwa hiyo, ujumbe wa Yawe, Mungu wa Israeli, ni huu: Niliahidi kwamba jamaa yako na jamaa ya babu yako mutakuja mbele yangu kunitumikia milele; lakini sasa jambo hilo likuwe mbali nami. Nitawaheshimu wale wanaoniheshimu, na wale wanaonizarau, nitawazarau. –Ni ujumbe wa Yawe.–