Nehemia 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 200226 Si Solomono alitenda zambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Yeye alikuwa mufalme mukubwa kuliko wafalme wa mataifa mengine. Mungu akamupenda na akamufanya kuwa mufalme juu ya watu wote wa Israeli, hata hivyo wanawake wa mataifa mengine, wakamusukuma kutenda zambi. Faic an caibideil |
Solomono alikuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli, na hawa ndio walikuwa wakubwa wa serikali yake wenye vyeo vya juu: Azariya mwana wa Zadoki alikuwa kuhani. Elihorefu na Ahiya, wana wa Sisa, walikuwa wakatibu. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa waaskari. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani. Azariya mwana wa Natani alikuwa mukubwa wa maliwali. Kuhani Zabudi mwana wa Natani alikuwa rafiki ya mufalme. Ahisari alikuwa mukubwa wa nyumba ya mufalme. Adoniramu mwana wa Abuda alikuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa.