Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 13:26 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

26 Si Solomono alitenda zambi kwa sababu ya wanawake wa namna hiyo? Yeye alikuwa mufalme mukubwa kuliko wafalme wa mataifa mengine. Mungu akamupenda na akamufanya kuwa mufalme juu ya watu wote wa Israeli, hata hivyo wanawake wa mataifa mengine, wakamusukuma kutenda zambi.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 13:26
10 Iomraidhean Croise  

Hakuna mutu aliyekusudia kutenda maovu mbele ya Yawe kama Ahabu, ambaye alishawishiwa na Yezebeli, muke wake.


basi, sasa ninakutimizia kama ulivyoomba. Ninakupa hekima na akili kwa kipimo ambacho hakuna mutu mwingine aliyepata kuwa nacho mbele yako, na wala hakutatokea mwingine kama wewe nyuma yako.


Vilevile, nitakupa yale ambayo haukuomba: nitakupa utajiri na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote wa nyakati zako.


Solomono alikuwa mufalme wa inchi yote ya Israeli, na hawa ndio walikuwa wakubwa wa serikali yake wenye vyeo vya juu: Azariya mwana wa Zadoki alikuwa kuhani. Elihorefu na Ahiya, wana wa Sisa, walikuwa wakatibu. Yosafati mwana wa Ahiludi alikuwa mwandishi wa habari. Benaya mwana wa Yehoyada alikuwa jemadari wa waaskari. Zadoki na Abiatari walikuwa makuhani. Azariya mwana wa Natani alikuwa mukubwa wa maliwali. Kuhani Zabudi mwana wa Natani alikuwa rafiki ya mufalme. Ahisari alikuwa mukubwa wa nyumba ya mufalme. Adoniramu mwana wa Abuda alikuwa musimamizi wa kazi za kulazimishwa.


ninakupa hekima na maarifa. Vilevile, nitakupa utajiri, mali na heshima zaidi ya mufalme mwingine yeyote aliyekuwa mbele yako na mufalme mwingine yeyote atakayetawala nyuma yako.”


Hivyo basi, mufalme Solomono aliwapita wafalme wote katika dunia kwa mali na kwa hekima.


Usimalize nguvu zako kwa wanawake, usiwape mali yako wale wanaoangamiza wafalme.


Jambo moja nililotambua linalokuwa baya zaidi kuliko kifo, ni mwanamuke ambaye moyo wake ni mutego na wavu, na mikono yake ni kama minyororo. Lakini anayemupendeza Mungu anamwepuka mwanamuke yule, lakini mwenye zambi ananaswa naye.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan