Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 13:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Watu wengine toka muji wa Tiro walileta samaki na biashara nyingine Yerusalema na kuwauzishia watu wetu siku ya Sabato.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 13:16
5 Iomraidhean Croise  

Wakati uleule, nikawaona watu wa Yuda wakikamua zabibu katika vikamulio siku za Sabato. Tena wengine walikuwa wakiwabebesha punda wao ngano, divai, zabibu, tini na vitu vingine wakivipeleka Yerusalema. Nikawaonya kwamba hawana ruhusa ya kuuzisha katika siku hiyo.


Nikawakaripia viongozi wa watu wa Yuda, nikisema: “Uovu gani huu munaofanya, kuichafua siku ya Sabato?


Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala nyama wako wa kufugwa, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako.


Kwa siku sita utafanya kazi zako, lakini siku ya saba utapumzika, kusudi ngombe wako na punda wako vilevile wapate kupumzika, na watoto wa mujakazi wako na wageni wapate kustarehe.


Lakini siku ya saba ni Sabato ya Yawe, Mungu wako. Siku hiyo usifanye kazi yoyote, wewe, wala mwana wako, wala binti yako, wala mutumwa wako, wala mujakazi wako, wala ngombe wako, wala punda wako, wala nyama wako yeyote, wala mugeni anayekuwa katika nyumba yako, kusudi mutumwa wako na mujakazi wako wapate kupumzika vilevile kama vile wewe.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan