Nehemia 13:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
1 Katika siku ile ya sherehe, kitabu cha Musa kikasomwa na ikajulikana kwamba Waamoni na Wamoabu hawaruhusiwi kuingia katika mukutano wa watu wa Mungu.
Naye mufalme akaenda katika nyumba ya Yawe pamoja na watu wote wa Yuda na wakaaji wote wa Yerusalema, na makuhani pamoja na manabii, watu wote, wadogo kwa wakubwa. Basi, akawasomea maneno ya kitabu cha agano kilichopatikana katika nyumba ya Yawe.
Lakini Sanibalati wa muji wa Muhori na Tobia, Mwamoni, mutumishi wake, waliposikia kwamba nimekuja kwa kushugulikia hali njema ya watu wa Israeli, hawakufurahia kabisa jambo hilo.
Lakini Sanibalati, Muhori, Tobia, Mwamoni mutumishi wake, na Gesemi, Mwarabu, waliposikia hayo, wakatucheka na kutuzomea wakisema: “Ni kitu gani hiki munachotenda? Munataka kumwasi mufalme?”
Ezra, ambaye alikuwa kuhani, akaenda na kuleta kitabu cha Sheria ya Musa mbele ya mukutano wote, wanaume na wanawake na yeyote aliyeweza kuelewa ile sheria. Siku hiyo ilikuwa ni siku ya kwanza ya mwezi wa saba.
Kwa muda wa yapata saa tatu, walisimama wakati Sheria ya Yawe, Mungu wao, ikisomwa. Na kwa saa tatu zilizofuata, walikuwa wakitubu na kumwabudu Yawe, Mungu wao.
Musome katika kitabu cha Yawe: Hakuna hata kiumbe kimoja kitakachokosekana, kila kimoja kitakuwa na mwenzake. Maana kinywa cha Yawe kimeamuru hivyo. Roho yake itawakusanya hao wote.
Juu ya inchi ya Moabu, Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Ole kwa watu wa Nebo, maana muji wao umeharibiwa! Kiriataimu umepatishwa haya, umetekwa, ukuta wake umebomolewa;
Yawe anasema hivi: Kwa sababu ya makosa matatu ya watu wa Amoni, hata kwa mane, sitageuza nia yangu. Katika vita yao kwa kupanua inchi, walipasua tumbo za wanawake wenye mimba katika inchi ya Gileadi.
akapeleka ujumbe kwa Balamu mwana wa Beori, huko Petori, karibu na muto Furati katika inchi ya Amawi. Akamwambia Balamu hivi: Kuna taifa ambalo limetoka Misri, nalo limeenea kila pahali katika inchi, tena linatishia kutwaa inchi yangu.
Na nyuma ya kusoma katika vitabu vya Sheria na vya manabii, wakubwa wa ile nyumba ya kuabudia wakatuma mutu kwa kuwaambia: “Wandugu, ikiwa muko na maneno ya kuwatia watu moyo, muyaseme.”