Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 11:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Kisha, viongozi wa watu wakakaa katika Yerusalema; watu wengine wote, wakapiga kura kati ya kila jamaa kumi kwa kuchagua jamaa moja itakayokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu. Jamaa zingine tisa zikakaa katika miji yao mingine.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 11:1
21 Iomraidhean Croise  

Kila jamaa, bila kujali wingi ilipiga kura kwa kuchagua mulango watakaosimamia.


Hao ndio waliokuwa wakubwa wa ukoo zao kulingana na vizazi vyao. Walikuwa wanaishi Yerusalema.


Hivi, Waisraeli wote walihesabiwa kufuatana na vizazi vyao na kuandikwa katika Kitabu cha Wafalme wa Israeli. Watu wa Yuda wamepelekwa katika utumwa mpaka Babeli kwa sababu ya kutokuwa waaminifu.


Watu wa kwanza kurudia katika miji ya inchi yao walikuwa Waisraeli wa kawaida, makuhani, Walawi na watumishi wa hekalu.


Wamoja kati ya watu wa makabila ya Yuda, Benjamina, ya Efuraimu na Manase walikwenda kuishi Yerusalema:


kwa ajili ya mikate mitakatifu, sadaka za unga za kawaida, sadaka za kuteketezwa kwa moto za kawaida, sadaka za siku za Sabato, sikukuu za mwandamo wa mwezi, sikukuu nyingine zilizowekwa, vitu vingine vitakatifu, sadaka za kusamehewa zambi, kwa kuwafanyia upatanisho watu wa Israeli na kazi nyingine zozote za nyumba ya Mungu wetu.


Walawi wote waliokaa katika Yerusalema, muji mutakatifu, walikuwa mia mbili makumi munane na wane.


Humo kulikuwa viti vya kifalme kwa kuamua maneno, ndivyo viti vya ukoo wa Daudi.


Muuombee Yerusalema amani mukisema: “Wote wanaokupenda wakae katika amani!


Kura inapigwa kwa kujua yatakayotukia, lakini uamuzi ni wa Yawe.


Ninyi munaona utukufu kujiita watu wa muji mutakatifu, na kujidai kumutegemea Mungu wa Israeli, ambaye jina lake ni Yawe wa majeshi.


Amuka! Amuka! Ujipatie zile nguvu zako, ewe Sayuni! Uvae nguo yako nzuri, ewe Yerusalema, muji mutakatifu. Maana hawataingia tena kwako watu wasiotahiriwa na wachafu.


Wakatoka ndani ya makaburi, na nyuma ya kufufuka kwa Yesu, wakaingia katika muji mutakatifu Yerusalema, na watu wengi wakawaona.


Halafu Shetani akamupeleka katika Yerusalema, muji mutakatifu, akamusimamisha kwenye pembe la juu sana la hekalu, na kumwambia:


Kisha wakaomba wakisema: “Bwana, wewe unayejua yanayokuwa ndani ya mioyo ya watu wote, utuonyeshe ni nani uliyemuchagua kati ya hawa wawili


Halafu wakapiga kura, na kura ikamwangukia Matia. Naye akaongezwa katika kundi la wale mitume kumi na mumoja.


Kule Shilo, Yoshua akazipigia kura sehemu hizo mbele ya Yawe, akawagawanyia Waisraeli; kila kabila na sehemu yake.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan