Mara tu amri hii ilipotolewa, watu wa Israeli wakatoa kwa wingi, malimbuko ya ngano, divai, mafuta, asali na mazao mengine mbalimbali ya shamba, na vilevile sehemu moja ya kumi ya kila kitu.
Wakati ule wakachagua watu wa kuchunga vyumba vya gala ambamo matoleo kwa ajili ya hekalu yaliwekwa, malimbuko ya kwanza, zaka na kuyakusanya kutoka katika mashamba ya miji, kwa ajili ya makuhani na Walawi kama ilivyotakiwa na Sheria. Watu wote wakafurahia makuhani na Walawi waliotumika,
alimuruhusu Tobia kutumia chumba kikubwa ambamo pale mbele walikuwa wakiweka sadaka za unga, ubani, vyombo, zaka za unga, divai, mafuta; vitu hivyo vyote Waisraeli walivyoagizwa kutoa kwa Walawi, waimbaji, walinzi wa milango, na matoleo kwa makuhani.
Mulete katika gala yangu zaka yote, kusudi katika nyumba yangu kuwe chakula cha kutosha. Kisha munaweza kunijaribu. Munipime namna hiyo nanyi mutaona kama sitayafungua madirisha ya mbinguni na kuwatiririshia baraka tele.
maana kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli ni wangu. Wakati nilipowaua wazaliwa wa kwanza wote wa Wamisri nilijitakasia kila muzaliwa wa kwanza katika Israeli; kila muzaliwa wa kwanza wa mwanadamu hata wa nyama; wao watakuwa wangu. Mimi ni Yawe.
Vilevile huko mutapeleka sadaka zenu za kuteketezwa kwa moto na sadaka zingine, sehemu ya kumi za mazao yenu, matoleo yenu ya mapenzi na ya kutimiza kiapo, na wazaliwa wa kwanza wa ngombe na kondoo wenu.