Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 1:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Niliposikia hayo nikaikaa chini na kulia, nikaomboleza kwa siku za kutosha. Nikafunga kula na kumwomba Mungu wa mbinguni,

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 1:4
22 Iomraidhean Croise  

Daudi alimwomba Mungu kwa ajili ya mutoto yule. Akafunga kula chakula, akaingia ndani ya chumba chake, na usiku kucha akalala chini.


Wakati uliposikia niliyosema juu ya pahali hapa na juu ya wakaaji wake, kwamba watakuwa ukiwa na kulaaniwa, ulijuta na kunyenyekea mbele yangu, hata ukapasua nguo yako na kulia mbele yangu. Basi, nami vilevile nimekusikia.


Solomono alikuwa ametengeneza mimbari ya shaba ambayo aliweka katikati ya kiwanja. Urefu na upana wake ulikuwa metre mbili na sentimetre makumi mbili na tano, na urefu kwenda juu metre moja na sentimetre makumi mbili na tano. Akapanda juu ya mimbari na kupiga magoti mbele ya watu wote wa Israeli, akainua mikono yake kuelekea mbinguni.


Hivi ndivyo Kiro mufalme wa Persia anavyosema: Yawe, Mungu wa mbingu, amenipatia falme zote katika ulimwengu na ameniagiza nimujengee nyumba katika Yerusalema, huko Yuda.


Wakati Ezra alipokuwa anaomba na kuungama naye akilia na kujiangusha uso mpaka chini mbele ya nyumba ya Mungu, kundi kubwa la watu wa Israeli, wanaume, wanawake na watoto, wakakusanyika karibu naye wakilia kwa uchungu mwingi.


Nilipoyasikia maelezo hayo, nikapasua nguo zangu na koti langu, nikaongoa nywele zangu na ndevu zangu kwa huzuni kubwa na kuikaa chini na kufazaika.


Magaribi, wakati wa kutoa sadaka ulipofika, nikasimama pahali pale nilipokuwa nimeikaa kwa huzuni nazo nguo zangu zimepasuka pamoja na koti, nikapiga magoti na kunyoosha mikono yangu kwa Yawe, Mungu wangu, na kuomba,


Nikawajibu: “Mungu wa mbinguni atatufanikisha katika kazi hii, nasi tunaokuwa watumishi wake tutaanza kujenga. Lakini ninyi hamuna sehemu au haki wala ukumbusho katika Yerusalema.”


Halafu mufalme Artasasta akanijibu: “Sasa unaomba nini?” Nikamwomba Mungu wa mbinguni.


Watumishi wako wanapenda muji ule, ijapokuwa ni mabomoko sasa; wanauonea huruma, ingawa umeharibika kabisa.


Mumushukuru Mungu wa mbinguni. Wema wake unadumu milele!


kandokando ya mito ya Babeli tuliikaa tukilia, tulipokumbuka Sayuni.


Wakati huo, mimi Danieli, nilikuwa nikiomboleza kwa muda wa majuma matatu.


Aliwaambia wamwombe Mungu wa mbinguni awaonee huruma juu ya fumbo hilo, kusudi wao wasiangamie pamoja na wenye hekima wengine wa Babeli.


Nilimwomba Yawe, kwa moyo, nikimutolea maombi pamoja na kufunga kula chakula, nikavaa gunia na kuikaa kwenye majivu.


Yona akawajibu: Mimi ni Mwebrania; ninamwabudu Yawe, Mungu wa mbingu, muumba wa bahari na inchi kavu.


kama vile katika siku ya sikukuu. Yawe anasema: Nitakuondolea hasara zako, nawe hautahitaji kupata haya kwa ajili yake.


Mufurahi pamoja na wenye kufurahi. Mulie pamoja na wenye kulia.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan