Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Nehemia 1:3 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

3 Wao wakaniambia: “Wayuda walioponyoka na kubaki katika jimbo lile, wako katika taabu nao wanazarauliwa. Ukuta wa Yerusalema umebomolewa na milango yake imeteketezwa.”

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Nehemia 1:3
33 Iomraidhean Croise  

basi, nitawahamisha watu wangu, Waisraeli, kutoka inchi hii ambayo nimewapa; vilevile na nyumba hii ambayo niliyoitakasa kwa ajili ya jina langu, nitaitupilia mbali nami, na kuifanya kitu cha kuchekelewa na kuzarauliwa kati ya watu wa mataifa yote.


Nao waaskari wote wa Babeli waliokuwa pamoja na mukubwa wa waaskari na walinzi wa mufalme walizibomoa kuta zilizouzunguka Yerusalema.


Aliichoma moto nyumba ya Mungu, akaubomoa ukuta wa Yerusalema, akazichoma moto nyumba zote za kifalme na kuharibu vyombo vyake vyote vya bei kali.


Hawa ndio watu wa majimbo waliotoka katika utumwa ambao Nebukadneza mufalme wa Babeli aliwapeleka wafungwa Babeli, wakarudi katika Yerusalema katika inchi ya Yuda. Kila mutu alirudi katika muji wake.


Tungetaka kukufahamisha, ee mufalme, kwamba tulikwenda katika jimbo la Yuda kunapokuwa nyumba ya Mungu Mukubwa. Nyumba hii inajengwa upya kwa mawe makubwamakubwa na kuta zake zinawekwa nguzo za miti. Kazi hiyo inafanywa kwa uangalifu mukubwa na inaendelea vizuri sana.


Na katika miji mingine, watu wa Israeli, makuhani, Walawi, walinzi wa milango na wazao wa watumishi wa Solomono, walikaa katika maeneo yao wenyewe, katika miji yao.


Nikatoka nikipitia kwenye Mulango wa Bonde katika njia inayoelekea kwenye Kisima cha Joka na mulango wa Yalala; nikachunguza kuta za muji wa Yerusalema ambazo zilikuwa zimebomolewa pamoja na milango yake ambayo ilikuwa imeteketezwa kwa moto.


Kisha nikawaambia: “Bila shaka munaona magumu yetu kwamba muji wa Yerusalema ni mabomoko na milango yake imeteketezwa kwa moto. Basi, tujenge tena ukuta wa Yerusalema kusudi tusifezeheshwe zaidi.”


Nikamujibu: “Ee mufalme, uishi milele! Kwa nini nisikuwe mwenye huzuni wakati Yerusalema ambamo makaburi ya babu zangu uko tupu na milango yake imeteketezwa kwa moto?”


Wale waliokuwa katika uhamisho kule Babeli, walirudi Yerusalema na katika inchi ya Yuda, kila mumoja akarudi katika muji wake. Jamaa zao walikuwa wamekaa Babeli tangu mufalme Nebukadneza alipowahamishia kule wakiwa watumwa.


Mufalme Ahasuero alipotawala ufalme wake ulikuwa na majimbo mia moja makumi mbili na saba, toka Uhindi mpaka Etiopia.


Tunazarauliwa na mataifa jirani, jirani zetu wanatuchekelea na kutusimanga.


Mutu asiyeweza kuzuia hasira yake ni kama muji usiokuwa na ulinzi unaposhambuliwa.


Kwa hiyo niliwazaraulisha wakubwa wa Pahali Patakatifu nikawaacha watu wa Yakobo waangamizwe, nikawaacha Waisraeli watukaniwe.


Na sasa nitawaambia jinsi nitakavyolifanya hilo shamba langu. Nitaubomoa upango wake, nalo litaharibiwa. Nitaubomoa ukuta wake, nalo litakanyagwakanyagwa.


Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza mbele ya falme zote za dunia. Watakuwa kitu cha zihaka, kitu cha kuzomewa, kuchekelewa na kulaaniwa kila fasi nitakapowasambaza.


Nitawashambulia kwa vita, njaa na magonjwa makali. Nitawafanya kuwa kitu cha kuchukiza kwa falme zote za dunia; nitawafanya kuwa mufano wa kutumia kwa kutoa laana. Mutakuwa kitu cha kushangaza, cha kuzarauliwa na cha kuzomewa kati ya mataifa yote nitakapowasambaza.


Wakaldea waliichoma kwa moto nyumba ya kifalme na nyumba za watu; vilevile walizibomoa kuta za Yerusalema.


Maana Yawe wa majeshi, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama vile hasira yangu na kasirani yangu ilivyowapata wakaaji wa Yerusalema, ndivyo kasirani yangu itakavyowapata ninyi, kama mutakwenda Misri. Mutakuwa kitu cha kutukaniwa, kitisho, laana na haya. Hamutaona tena nafasi hii.


Mupande, mupite katika mashamba yake ya mizabibu, muharibu kila kitu lakini musivimalize kabisa. Mukate matawi yake, kwa maana hayo si yangu mimi Yawe.


Waaskari wote wa Wakaldea waliokuwa pamoja na mukubwa wa waaskari, walizibomoa kuta zote zilizouzunguka Yerusalema.


Unapokuwa sasa mabomoko matupu, Yerusalema unakumbuka utukufu wake. Ulipoangukia katika mikono ya waadui zake, hakuna aliyekuwa pale kwa kuusaidia. Washindi wake walichekelea kuanguka kwake.


Milango yake imezama ndani ya udongo, ameharibu na kuvunjavunja vifungio vyake. Mufalme na wakubwa wake wako katika uhamisho kati ya mataifa. Hakuna sheria tena, manabii wake hawapati tena maono kutoka kwa Yawe.


Umesikia matukano yao, ee Yawe, na mipango yao yote juu yangu.


Ukumbuke, ee Yawe, mambo yaliyotupata! Utuangalie, uone haya yetu!


Miji yenu nitaiteketeza, pahali penu patakatifu nitapafanya jangwa na harufu zenu nzuri za sadaka sitazikubali.


Nitawatawanya ninyi kati ya watu wa mataifa na kuchomoa upanga juu yenu. Inchi yenu itakuwa ni ukiwa na miji yenu uharibifu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan