4 Lakini anayeambatana na wanaoishi angali bado na tumaini. Afazali imbwa mwenye kuishi kuliko simba mwenye kufa.
Asiyemwogopa Mungu ana tumaini gani wakati Mungu anapokata pumzi yake, anapomwondolea uzima wake?
Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.
Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.
Huko kuzimu mutu hawezi kukushukuru wewe; waliokufa hawawezi kukushukuru wewe. Wala wanaoshuka kule katika shimo hawawezi tena kutumainia uaminifu wako.