17 Afazali kusikiliza maneno matulivu ya mwenye hekima, kuliko kusikiliza kelele za mufalme katika kikao cha wapumbafu.
Anayemwonya mwenzake kwa mwisho atasifiwa naye, kuliko yule anayemubembeleza kwa maneno matamu.
Maneno ya mwenye hekima yanamupa upendeleo; lakini maneno ya mupumbafu yanamwangamiza.
Afazali kusikia maonyo ya wenye hekima kuliko kusikiliza nyimbo za wapumbafu.
Hatalalamika wala hatapiga kelele, wala hatasema kwa sauti kubwa katika barabara.
Yeye hataregea wala kuchoka, mpaka atakapoimarisha sheria yangu katika dunia. Watu wa mbali wanangojea mafundisho yake.
Kisha kusema maneno haya, akaaga mukutano.
Kwa maana mutu mwenye kasirani hawezi kutimiza mambo ya haki mbele ya Mungu.