16 Basi, mimi ninasema, hekima ni bora kuliko nguvu, ingawa hekima ya masikini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.
Mali ya tajiri ndiyo kikingio chake. Umasikini wa masikini unamuletea maangamizi.
Mwenye hekima anaweza kuteka muji wa wenye nguvu na kukiporomosha kikingio wanachokitegemea.
Kuwa na hekima na maarifa ni bora kuliko kuwa na nguvu.
Nina uwezo wa kushauri na kuamua vizuri. Nina ufahamu na nina nguvu.
Nguvu nyingi zaidi zinahitajika kwa mutumiaji wa shoka lisilonolewa, lakini kutumia hekima kunamufanya mutu afanikiwe.
Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.
Hekima inamufanya mwenye hekima kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi katika muji.
Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.