Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 9:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 9:12
28 Iomraidhean Croise  

Atawanyeshea waovu makaa ya moto na kiberiti; upepo mukali utakuwa ndio azabu yao.


maana maangamizi yatawatokea kwa rafla. Hakuna anayejua magumu watakayoleta.


Mutu mubaya ananaswa kwa kosa lake, lakini mutu wa haki anaimba na kufurahi.


Kutokana na hayo hasara itamupata kwa rafla; kwa rafla atapondekana vibaya wala hatapata kupona.


Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.


Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.


Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.


Vilevile hapa chini ya jua nimeona mufano wa hekima, na ulionekana kwangu kuwa wenye maana sana.


Mutu atakayekimbia sauti ya woga atatumbukia ndani ya shimo; na mutu atakayetoka ndani ya shimo atanaswa katika mutego. Madirisha ya mbinguni yamefunguliwa, misingi ya dunia inatikisika.


Basi, zambi hii itakuwa kwenu kama ufa mukubwa katika ukuta murefu; utabomoka mara moja na kuanguka chini kwa rafla.


Bwana wetu Yawe anasema: Nitautupa wavu wangu juu yako, nao watu watakuvua humo kwa wavu wangu.


Watakapokwenda nitatandaza wavu wangu niwanase, nitawaangusha chini kama ndege toka katika anga; nitamwaazibu kufuatana na jinsi walivyotangaza kwa kusanyiko lao.


Nabii ni mulinzi wa Waefuraimu kwa pahali pa Mungu; lakini, popote anapoenda anategewa mutego kama ndege. Hata katika nyumba ya Mungu wake anachukiwa.


Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Munajua vema kwamba mwenye nyumba angejua saa gani mwizi atakapokuja kumwiba, asingeacha nyumba yake ibomolewe.


Kwa maana Mungu anasema hivi katika Maandiko Matakatifu: “Kwa wakati uliofaa, nilijibu maombi yako. Kwa siku ya wokovu, nilikusaidia.” Basi sasa, huu ndio wakati unaofaa, sasa leo ni siku ya wokovu.


Watu watakapokuwa wakisema: “Kuna amani na usalama”, ndio wakati uharibifu utakapowapata kwa rafla kama vile maumivu ya kuzaa yanavyomupata mwanamuke mwenye mimba, wala hawataweza kuponyoka.


Kwa njia hiyo wanaweza tena kupata ufahamu na kuponyoka katika mitego ya Shetani, aliyewanasa na kuwafanya watimize mapenzi yake.


Mukuwe na mwenendo muzuri kati ya wapagani, kusudi wakiwasingizia kwamba mumefanya mabaya, wapate kuona matendo yenu mema na wamutukuze Mungu siku ile ya kuja kwake.


Walimu hawa wa uongo ni kama nyama wasiokuwa na akili ambao wanazaliwa tu kwa kunaswa na kuchinjwa. Wao wanasema vibaya juu ya mambo yote wasiyojua. Wataangamizwa kufuatana na ubaya wao wenyewe.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan