Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 9:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Kila kitu unachotaka kufanya ukifanye kwa nguvu zako zote, maana, hakuna kazi, wala wazo, wala maarifa, wala hekima kule katika kuzimu unakokwenda.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 9:10
44 Iomraidhean Croise  

Watoto wake wanaume na wanawake wakamufikia kwa kumufariji, lakini akakataa kufarijiwa, akisema: “Uniache. Nitaendelea kuomboleza kwa ajili ya mwana wangu, mpaka nitakaposhuka katika kaburi.” Ndivyo baba yake alivyomulilia.


Sasa, mumutumikie Yawe, Mungu wenu, kwa nia na moyo wote. Basi mujitayarishe kumujengea Yawe pahali patakatifu kusudi Sanduku la Agano la Yawe pamoja na vyombo vyote vitakatifu vinavyotumiwa katika ibada, viwekwe ndani ya nyumba iliyojengwa kwa ajili ya Yawe.”


Kisha, mufalme Daudi akamwambia Solomono mwana wake: “Uwe imara na hodari, ufanye kazi hii. Usiogope wala kuwa na wasiwasi. Yawe Mungu ambaye ni Mungu wangu, yuko pamoja nawe. Hatakuachilia lakini atakuwa nawe mpaka itakapomalizika kazi yote ambayo inayohitajika kufanyiwa kwa nyumba ya Yawe.


Kisha nikaondoka usiku, mimi pamoja na watu wachache; sikumwambia mutu yeyote yale ambayo Mungu alikuwa ameyaweka ndani ya moyo wangu kwa ajili ya Yerusalema. Lakini siku moja usiku, nikaondoka na kutwaa watu wachache tu. Sikupeleka nyama yeyote isipokuwa punda niliyepanda juu yake mimi mwenyewe.


Kwa hiyo wakafanya shauri baya kwa kuja pamoja Yerusalema kutushambulia na hivyo kuleta muvurugano katika muji ule.


Wayuda waliokaa kati ya waadui zetu waliposikia maneno yao, mara kwa mara, walitufikia mara kumi wakisema: “Watakuja toka kila pahali wanapokaa na kutushambulia.”


mbele ya kwenda kule ambako sitarudi, kule kwenye inchi ya huzuni na giza kubwa;


inchi ya huzuni na fujo, ambako mwangaza wake ni kama giza.


Wanaishi maisha ya fanaka kisha wanashuka kwa amani katika kuzimu.


Unigeukie, ee Yawe, uniokoe; uniponyeshe kwa sababu ya wema wako.


Usimwambie jirani yako “Kwenda na urudie kesho, halafu nitakupatia” wakati wewe unaweza kumupa anachohitaji leo.


Mawingu yakijaa maji, mvua inanyesha. Muti ukiangukia upande wa kusini au wa kaskazini, pale unapoangukia ndipo unapolala.


Panda mbegu asubui na usiache kupanda mpaka magaribi, maana, haujui mbegu gani zitaota; za asubui, za magaribi, au zote zitakuwa nzuri.


Nilisema: nikiwa mubichi kabisa, inanipasa niage dunia. Mimi nimepangiwa kwenda katika kuzimu siku zote zilizonibakilia.


Mutanitafuta mimi na kuniona. Mutakaponitafuta kwa moyo wote,


Lakini Kalebu akanyamazisha watu mbele ya Musa, akasema: Tuende mara moja tuitwae inchi hiyo. Kwa sababu tuko na uwezo sana wa kushinda.


Nao wakamujibu: ‘Kwa sababu hakuna mutu aliyetupatia kazi.’ Halafu akawaambia: ‘Ninyi vilevile muende kutumika katika shamba langu la mizabibu.’


Lakini ninyi mushugulikie kwanza Ufalme wa Mungu na kufuata haki mbele yake, naye atawaongezea vitu vile vyote.


Yesu akawaambia: “Chakula changu ni kufanya mapenzi ya yule aliyenituma na kutimiza kazi yake.


kwa sababu malaika wa Bwana alishuka mara kwa mara ndani ya kile kisima na kutikisa maji. Na mugonjwa wa kwanza aliyeingia ndani ya maji kisha kuyatikisa, alipona ugonjwa wowote aliokuwa nao.]


Imetupasa kufanya kazi za yule aliyenituma wakati kungali muchana, kwa sababu usiku unakaribia, wakati mutu asipoweza kutumika.


Musikuwe wavivu katika kazi lakini mukuwe na bidii, mukimutumikia Bwana kwa juhudi.


Lakini kwa neema ya Mungu nimekuwa sawa hivi ninavyokuwa, na neema yake niliyopewa haikukuwa ya bure, lakini nilitumika zaidi sana kuliko mitume wote wengine. Hakika si mimi, lakini ni neema ya Mungu inayokuwa pamoja nami.


Kama Timoteo akifika, mujikaze kumupokea vizuri kati yenu kwa sababu yeye anafanya kazi ya Bwana kama mimi mwenyewe.


Munajua hakika kuwa wale wanaofanya mashindano ya kukimbia, wote wanakimbia lakini ni mumoja tu anayepokea zawadi. Basi mukimbie hata mufikie kupokea zawadi.


Ni kwa sababu hiyo ninakimbia nikiwa na shabaha ya kushinda. Mimi ni kama mupiganaji wa ngumi asiyepiga katika hewa.


Mutumie vema wakati huu munaokuwa nao kwa maana siku hizi ni mbaya.


Na kila kitu munachofanya, mukifanye kwa moyo wenu wote, kama vile wenye kumutumikia Bwana wala si watu.


Wakati mambo haya yatakapokutokea, chochote utakachoweza kufanya ukifanye, maana Mungu yuko pamoja nawe.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan