Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Hakuna mutu anayekuwa na uwezo wa kushikilia roho yake kusudi asikufe; hakuna mutu anayekuwa na uwezo juu ya siku ya kufa. Wakati wa vita hakuna kuponyoka, na uovu hauwezi kumwokoa mwovu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:8
21 Iomraidhean Croise  

Sisi wote tutakufa. Sisi ni kama maji yaliyomwangika chini ambayo hayawezi kuzoleka. Lakini Mungu hataki Abusaloma akufe sasa au aendelee kuishi mbali naye.


Watu hao wakaenda mpaka Yordani na katika njia waliona nguo na vifaa vingine Waaramu walivyoacha walipokuwa wanakimbia. Wakarudi na kumupasha mufalme habari.


Siku za kuishi za mwanadamu zimepimwa. Ee Mungu, umepanga hesabu ya miezi yake; hawezi kupita mupaka uliomwekea.


Kama Mungu angejifikiri tu yeye mwenyewe, akiondoa pumzi yake ya uzima katika dunia,


Unikumbuke, ee Bwana. Maisha ni mafupi! Umewaumba wanadamu wote kwa bure?


Yawe amejitambulisha; anatoa hukumu. Waovu wamenaswa kwa matendo yao wenyewe.


Mutu hawezi kudumu katika kutenda maovu, lakini hakuna kitu kinachoweza kumwangusha mutu wa haki.


Mwovu anaangamizwa kwa matendo yake maovu, lakini mwenye haki atapata usalama kwa uaminifu wake.


Nani anayejua, basi, kama kweli roho ya mutu inapanda juu, na roho ya nyama inashuka chini ndani ya udongo?


Lakini hakuna furaha kwa waovu. Wao watapita kama kivuli, maisha yao hayatakuwa marefu kwa sababu hawamwogopi Mungu.


Mutu hajui saa yake itafika wakati gani. Kama vile samaki wanavyonaswa katika wavu kwa bahati mbaya, na kama vile ndege wanavyonaswa katika mutego kwa rafla, ndivyo wanadamu wanavyonaswa na hasara inapowaangukia bila kutazamia.


Ninyi munajidai mumefanya agano na kifo mumefanya mapatano na kuzimu! Ninyi munasema kwamba hasara itakapokuja haitawapata, kwa sababu mumefanya uongo kuwa tegemeo lenu, na udanganyifu kuwa kikingio chenu!


Halafu agano lenu na kifo litavunjika, na mapatano yenu na kuzimu yatafutwa. Ile hasara kubwa itakapokuja itawaangusha chini.


Ulijiona salama katika uovu wako; ukajisemesha: Hakuna mutu anayeniona. Hekima na elimu yako vilikupotosha, ukajisemesha ndani ya moyo wako: Mimi ndiye; hakuna mwingine isipokuwa mimi.


na hali ya utukufu; nao unazikwa katika uzaifu, lakini unafufuka na nguvu.


Ni kweli Kristo alitundikwa juu ya musalaba katika hali ya uzaifu wa mwili, lakini sasa anaishi kwa uwezo wa Mungu. Nasi katika kuungana kwetu naye sisi vilevile tunakuwa zaifu. Lakini kwa ajili yenu tunaishi pamoja naye kwa nguvu ya Mungu.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan