Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:17 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

17 lakini hataelewa kazi ya Mungu inayofanyika chini ya jua. Mutu anaweza kutoa jasho sana lakini hataelewa. Wenye hekima wanaweza kujidai kwamba wanajua, lakini, kwa kweli, hawajui.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:17
13 Iomraidhean Croise  

yeye anayetenda mambo makubwa yasiyochunguzika, anayetenda maajabu yasiyohesabika.


Ee Yawe, matendo yako ni mengi sana! Umeyafanya kwa hekima yote! Dunia imejaa viumbe vyako!


Heri mutu anayemutumainia Yawe, mutu asiyejiunga na watu wenye majivuno, watu waliopotoka kwa kuabudu miungu ya uongo.


Basi, nilijaribu kufikiri juu ya jambo hili, lakini lilikuwa gumu sana kwangu,


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Kama vile hauwezi kujua jinsi uzima unavyoingia katika mifupa ya mutoto katika tumbo la mama yake, vilevile hauwezi kuelewa matendo ya Mungu, aliyefanya kila kitu.


Mungu amefanya kila kitu kikuwe kizuri kwa wakati wake. Ameweka ndani ya moyo wa mwanadamu mawazo juu ya muda usiokuwa na mwisho, lakini mutu hawezi kuelewa mwanzo na mwisho wa matendo ya Mungu.


Mufikiri vema juu ya kazi ya Mungu. Ni nani anayeweza kunyoosha kitu Mungu alichokunja?


Ninyi hamujui bado? Hamujapata kusikia? Yawe ndiye Mungu wa milele; yeye ndiye Muumba wa kila kitu katika dunia. Yeye haregei hata kidogo wala kuchoka. Maarifa yake hayachunguziki.


Utajiri wa Mungu, hekima na ufahamu wake ni vikubwa kupita kipimo! Hakuna anayeweza kuvumbua kusudi lake wala kuelewa mipango yake!


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan