Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:16 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

16 Kila mara nilipojitoa kwa kujua hekima na kuona yanayotendeka hapa katika dunia, nilitambua kwamba mutu anaweza kukaa macho muchana na usiku,

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:16
11 Iomraidhean Croise  

Hivyo, muchana nilivumilia jua kali na usiku baridi ilinipiga. Sikuweza kupata usingizi hata kidogo.


Munajisumbua bure kuamuka asubui mapema na kuchelewa kwenda kupumzika magaribi, mujipatie chakula kwa jasho lenu. Mungu anatimiza mahitaji ya wapendwa wake hata wanapolala.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!


Nilifanya bidii kujua umbalimbali kati ya hekima, wazimu na upumbafu. Lakini niligundua kwamba kufanya hivyo ni sawa na kutaka kukamata upepo.


Maisha yake yote yamejaa taabu, na jasho yake ni mahangaiko matupu. Hata usiku akili yake haipumziki! Hayo nayo ni bure.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Tena, nimeona jambo moja ovu sana chini ya jua: mutu alijikusanyia mali, ikakuwa hatari kwake.


Hata hivyo, nilikusudia kujua na kuchunguza na kutafuta hekima na maana ya mambo yanayokuwa, na vilevile kujua kwamba uovu ni upumbafu na kwamba upumbafu ni wazimu.


Hajui ni kitu gani kitakachotukia nyuma, maana ni nani anayeweza kumujulisha yatakayotukia nyuma?


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan