Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

11 Kwa vile uovu hauazibiwi haraka, mioyo ya wanadamu inakusudia kutenda mabaya.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:11
19 Iomraidhean Croise  

Katika barua hiyo Daudi aliandika hivi: “Umuweke Uria kwenye mustari wa mbele, pahali ambako mapigano ni makali kabisa, kisha umwache kule na kurudia nyuma kusudi apigwe, na akufe.”


Anawaacha waovu wajione salama, lakini macho yake yanachunguza mienendo yao.


Katika majivuno yake anasema: “Mungu hatagundua. Hakuna Mungu.” Hayo ndiyo mawazo yake yote.


Anawaza ndani ya moyo: “Sitakuwa na wasiwasi; sitapatwa na taabu katika maisha.”


Lakini wewe, Bwana, ni Mungu wa rehema na huruma; wewe ni muvumilivu, mwingi wa wema na uaminifu.


Kisha Yawe akapita mbele ya Musa akitangaza tena: Yawe, Yawe, ni Mungu mwenye rehema na huruma, si mwepesi wa hasira, ni mwingi wa wema na uaminifu.


Wale wachawi wakamwambia mufalme wa Misri: “Hii ni kazi ya mukono wa Mungu.” Lakini moyo wa mufalme ukaendelea kuwa mugumu, wala hakuwasikiliza Musa na Haruni. Ikakuwa kama vile Yawe alivyokuwa amesema.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Lakini waovu hata wakipewa rehema, hawawezi kujifunza kutenda haki. Hata katika inchi ya usawa, wao bado wanatenda maovu, wala hawajali ukubwa wako wewe Yawe.


Mulimwogopa na kutishwa na nani hata mukasema uongo, mukaacha kunikumbuka mimi na kuacha kabisa kufikiri juu yangu? Mimi sikuwaambia kitu kwa muda murefu; ndiyo maana labda mukaacha kuniheshimu!


basi, musikilize jinsi Yawe anavyosema enyi mabaki ya Yuda. Yawe, Mungu wa Israeli, anasema hivi: Kama mumekusudia kwenda katika inchi ya Misri na kukaa huko,


Moabu amestarehe tangu ujana wake, ametulia kama divai katika mutungi. Hajamimiliwa toka chombo kimoja katika chombo kingine, hajapata kupelekwa katika uhamisho. Kwa hiyo angali na onjo yake, harufu yake nzuri haijabadilika hata kidogo.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan