Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:10 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

10 Tena, nimeona waovu wakizikwa, watu ambao walizoea kuingia na kutoka pahali patakatifu, na kusifiwa katika muji uleule walimotenda maovu yao. Hayo nayo ni bure.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:10
14 Iomraidhean Croise  

Hata hivyo, wapeperushwe kama majani yenye kukauka, wakuwe kama maganda yanayopelekwa na zoruba!


Waadui zangu wote wananizarau, na hasa zaidi wenzangu. Warafiki zangu wameniona kuwa kitisho; wanaponiona katika njia wananikimbia.


Mwenye haki anakumbukwa kwa baraka, lakini waovu watasahauliwa kabisa.


Hakuna mutu anayekumbuka mambo ya zamani, wala atakayekumbuka yatakayotukia kisha.


Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!


Katika muji ule, kulikuwa masikini mumoja mwenye hekima ambaye, kwa hekima yake, aliokoa muji ule. Lakini hakuna mutu aliyemukumbuka yule masikini kisha.


Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.


Ee Yawe, tumaini la Waisraeli, wote wanaokukataa wafezeheshwe. Wanaokuacha wewe watatoweka, kama majina yaliyoandikwa chini katika mavumbi, kwa maana wamekuacha wewe Yawe, unayekuwa chemichemi ya maji ya uzima.


Siku moja yule masikini akakufa, na wamalaika wakamupeleka mpaka pembeni ya Abrahamu. Na yule tajiri akakufa vilevile na kuzikwa.


Kisha wakaleta washuhuda wa uongo waliosema: “Mutu huyu hachoki na kusema maneno ya kutukana hili hekalu letu takatifu pamoja na Sheria ya Musa!


Mwenye haki mbele yangu ataishi kwa njia ya imani. Lakini kama akirudi nyuma, sitapendezwa naye.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan