Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 8:1 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

1 Nani anayekuwa kama mwenye hekima? Nani anayejua maana ya kila kitu? Hekima inaangarisha uso wa mutu, inaondoa alama za upumbafu.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 8:1
27 Iomraidhean Croise  

Wakamujibu: “Tuna huzuni kwa sababu tumeota ndoto na hakuna anayeweza kututafsiria ndoto zetu.” Yosefu akawaambia: “Kutafsiri ndoto si kazi ya Mungu? Basi, muniambie ndoto zenu.”


Lakini inawezekana kwamba malaika, ambaye ni mupatanishi mumoja kati ya maelfu, atakuwa karibu na mutu yule kwa kumufunulia jambo la kufanya.


nao Waisraeli waliona uso wake unangaa. Halafu Musa alifunika tena uso wake kwa kitambaa mpaka alipokwenda kuongea na Yawe.


Wataweza kuelewa mezali na maana iliyofichwa, watayaelewa maneno ya wenye hekima na vitendawili vyao.


Mutu anasifiwa kadiri ya hekima yake, lakini mwenye moyo wa mafikiri mabaya anazaruliwa.


Hekima ni mbele ya uso wa mwenye akili, lakini macho ya mupumbafu yanaangalia kwa miisho ya dunia.


Mutu mwovu anajionyesha kuwa hodari, lakini mutu wa usawa anafikiri vizuri juu ya mwenendo wake.


Kuwa na hekima na maarifa ni bora kuliko kuwa na nguvu.


Anafunua siri na mafumbo, anajua kinachokuwa katika giza, mwangaza unakaa kwake.


Mufalme akamwambia Danieli: Hakika, Mungu wako ni Mungu wa miungu na Bwana wa wafalme, na ndiye anayefumbua mafumbo kwa sababu ameweza kunifumbulia fumbo hili.


Na kule sura ya Yesu ikageuka wazi mbele yao. Uso wake ukangaa kama jua, nazo nguo zake zikametameta kama mwangaza.


Wajumbe wa Baraza Kubwa walishangaa sana kuona namna Petro na Yoane walivyosema bila woga na kujua kwamba walikuwa watu wasiojulikana na wasiokuwa na elimu. Wakatambua kwamba walikuwa pamoja na Yesu.


Na sasa Ee Bwana, angalia vitisho vyao. Basi utuwezeshe sisi watumishi wako tupate kutangaza neno lako kwa uhodari kabisa.


Na wote waliohuzuria katika lile Baraza wakamukazia Stefano macho, wakaona uso wake unafanana sawa na uso wa malaika.


Kwa sababu hii ni lazima kuwatii wenye mamlaka, si kwa sababu ya kuogopa azabu ya Mungu tu, lakini tena kwa sababu ya kusongwa na zamiri.


Muniombee vilevile, kusudi Mungu anijalie maneno ya kusema. Kwa hiyo nitaweza kuwajulisha watu kwa uhodari siri ya Habari Njema.


Watu wa taifa hilo watakuwa na nyuso kali. Hawatajali wazee wala kuwahurumia vijana.


Lakini Bwana alinisaidia, akanitia nguvu nipate kuitangaza Habari Njema kwa ukamilifu kusudi watu wa mataifa mengine wapate kuisikia. Nami nikaokolewa toka katika kinywa cha simba.


Mbele ya yote, mujue kwamba hakuna mutu anayeweza kufasiria yeye mwenyewe unabii unaokuwa katika Maandiko Matakatifu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan