Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 7:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mwenye hekima akimutesa mutu, yeye anafanya kama mupumbafu. Kupokea kituliro kunapotosha akili.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 7:7
14 Iomraidhean Croise  

Usipokee kituliro, maana kituliro kinapofusha wakubwa na kupotosha mambo ya wenye haki.


Mutu mubaya anapokea kituliro kwa siri kusudi apate kupotosha haki.


Kwa anayetoa kituliro ni kama hirizi; kila kitu anachofanya yeye anafanikiwa.


Kisha nikaona mateso yote yanayofanyika chini ya jua. Watu wanaogandamizwa wanalia machozi, lakini hakuna mutu yeyote anayewafariji. Wagandamizaji wao wana nguvu, ndiyo sababu hakuna wa kuwafariji.


Faida ya mavuno ya inchi ni kwa watu wote, hata mufalme vilevile anatumainia mavuno yale.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Wakubwa wako ni waasi; wanashirikiana na wizi. Kila mumoja anapenda kituliro, na kukimbilia zawadi. Hawamupatii yatima haki yake, haki za wajane si kitu kwao.


Ni mutu anayekuwa hivi: anaishi kwa haki na kusema kwa usawa, anazarau kabisa utajiri wa unyanganyi, anakataa kupokea kituliro, hakubali hata kidogo kusikia mipango ya mauaji, wala hakubali macho yake yaone maovu.


Musipotoshe haki, musikuwe na upendeleo, wala musikubali kupokea kituliro, kwa kuwa kituliro kinapofusha macho ya watu wenye hekima na kupotosha maneno ya mutu mwenye haki.


Hamutakuwa na raha yoyote pahali penu wenyewe pa kutulia wala kati ya mataifa hayo. Lakini Yawe atawapa huko wasiwasi wa moyo, kufifia kwa macho na mahangaiko ya ndani ya roho.


Niko hapa, na kama nimefanya tendo lolote baya, basi, mutoe ushuhuda mbele ya Yawe na mbele ya mufalme wake muchaguliwa. Nimenyanganya ngombe dume au punda wa mutu yeyote? Nimemugandamiza mutu yeyote? Nimemutesa mutu yeyote? Nimepokea kituliro kwa mutu yeyote kusudi nifunge macho mbele ya matendo yake? Museme nami nitamurudishia kitu chochote kile.”


Hivyo, akabadilisha tabia yake, akijifanya mwenda-wazimu, akakuwa anakwaruzakwaruza kwenye milango ya muji, na kuacha mate yake yatiririke kwenye ndevu zake.


Lakini watoto hao hawakufuata mwenendo wa baba yao. Lakini walianza kujitafutia faida. Wakapokea kituliro na kupotosha haki.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan