Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 7:4 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

4 Moyo wa mwenye hekima uko ndani ya nyumba ya kilio, lakini moyo wa mupumbafu unapenda raha.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 7:4
21 Iomraidhean Croise  

Abusaloma akawaambia watumishi wake: “Mumwangalie Amunoni atakapokuwa amekunywa divai na kufurahi. Nitakapowaambia: ‘Mumupige Amunoni’, mumwue. Hiyo ni amri yangu kwenu. Mujipe moyo na mukuwe hodari.”


Basi, wakati wa saa sita za muchana, Beni-Hadadi na wale wafalme wenzake makumi tatu na wawili waliomwunga mukono walipokuwa katika mahema yao wakikunywa na kulewa, mashambulizi yakaanza.


Basi, nikawaza: “Ngoja nijitumbukize katika raha, nijifurahishe.” Lakini, niligundua kwamba hiyo nayo ni bure.


Huzuni ni afazali kuliko kicheko, maana, kwa huzuni ya uso moyo unafurahishwa.


Afazali kusikia maonyo ya wenye hekima kuliko kusikiliza nyimbo za wapumbafu.


Moyo unanidunda na woga umenishika. Nilitamani magaribi ifike, lakini ilipofika ikakuwa ya kutetemesha.


Wakiwa na hamu kubwa nitawatayarishia karamu: nitawalewesha mpaka wapepesuke; nao watalala usingizi wa siku zote na hawataamuka tena. –Ni ujumbe wa Yawe.–


Nitawalewesha wakubwa na wenye hekima wake, watawala wake, maliwali na waaskari wake; watalala usingizi wa milele wala hawataweza tena kuamuka. –Ni ujumbe wa mufalme, jina lake Yawe wa majeshi!


Usiku uleule, mufalme Belsasari wa Wakaldea, aliuawa.


Kwenye sikukuu ya mufalme, waliwalewesha sana wakubwa wake; naye mufalme akashirikiana na watu wa ovyoovyo.


Watateketezwa kama kichaka cha miiba, wao wanaoikalia kulewa. Watateketezwa kama vile majani yenye kukauka.


Abigaili aliporudi kwake, alimukuta Nabali akifanya karamu kubwa katika nyumba yake kama ya kifalme. Nabali alikuwa akifurahi sana ndani ya moyo maana alikuwa amelewa sana. Kwa hiyo hakumwambia neno lolote mpaka asubui.


Yule kijana alimwongoza Daudi mpaka kwenye kundi lile. Walipofika kule waliwakuta wanyanganyi wale wakiwa wametawanyika kila pahali maana walikuwa wakikula na kunywa kwa sababu vitu walivyonyanganya kutoka inchi ya Wafilistini na inchi ya Yuda vilikuwa vingi sana.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan