22 Wewe mwenyewe unajua ndani ya moyo kwamba umetukana wengine mara nyingi.
Mufalme aliendelea kumwambia Simei: “Unayajua wazi maovu uliyomutendea baba yangu Daudi. Sasa, kwa sababu ya hayo, Yawe atakuazibu.
Usifuate maneno yote wanadamu wanayosema, kusudi usisikie mutumishi wako akikutukana.
Nimeyapima yale yote kwa hekima; nikajisemesha: “Ninataka kuwa mwenye hekima!” Lakini hekima iko mbali sana nami.
Kwa maana ndani ya moyo munatoka mawazo mabaya yanayoleta uuaji, uzinzi, uasherati, wizi, ushuhuda wa uongo na matukano.
Kwa njia ya ulimi tunamusifu Bwana anayekuwa Baba yetu, na kwa njia ile ile tunalaani watu walioumbwa kwa mufano wa Mungu.