Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 7:2 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

2 Afazali kwenda kwenye kilio, kuliko kwenda kwenye karamu, kwa sababu inawapasa wenye kuwa wazima kukumbuka kwamba kifo kinawangojea sisi wote.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 7:2
29 Iomraidhean Croise  

Utufundishe ufupi wa maisha yetu kusudi tuweze kuwa na hekima.


Mwenye hekima anaona anakokwenda, lakini mupumbafu anatembea katika giza. Hata hivyo, ninajua vilevile kwamba mwisho wao wote wawili ni mumoja.


Maana hakuna anayemukumbuka mwenye hekima, wala anayemukumbuka mupumbafu, maana katika siku zinazokuja wote watasahaulika. Maana mwenye hekima anakufa sawasawa na mupumbafu!


Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.


Wote wanakufa na kwenda kwa nafasi moja. Wote wametoka katika mavumbi na wote watarudi katika mavumbi.


Ingawa mutu huyo ataishi miaka elfu mbili, lakini hafurahii maisha, basi yeye ni kama yule mutoto. Wote wawili wanakwenda fasi moja.


maana mwisho uleule unawapata wenye haki na waovu, wazuri na wabaya, wanaohesabiwa kuwa safi na wachafu, wenye kutoa sadaka na wasiotoa sadaka. Mutu muzuri ni sawa tu na mwenye zambi, na mwenye kuapa si tofauti na asiyeapa.


Hili ni jambo baya zaidi kati ya yote yanayotukia hapa chini ya jua, kwamba mwisho uleule unawapata wote. Tena, wakati wote wa maisha yao, wanadamu wanajaa uovu na wazimu, na kisha wanakufa.


Maana, wanaoishi wanajua kwamba watakufa, lakini wafu hawajui kitu chochote. Hawana malipo tena. Hakuna ukumbusho juu yao, wamesahauliwa kabisa.


Ulijisemesha ndani ya moyo: “Nitakuwa malkia milele”, nawe haukufikiri juu ya mambo yanayotokea, wala kuwaza juu ya mwisho wake.


Usiingie katika nyumba watu wanamofanya karamu. Usiikae kula na kunywa pamoja nao.


Basi, Yawe wa majeshi anasema hivi: Mufikiri vizuri juu ya namna munavyofanya!


Ni lazima muniheshimu mimi kwa matendo yenu. Musiponisikiliza nitawaletea laana. Vitu vyote munavyopewa kwa mahitaji yenu nitavilaani. Na kweli nimekwisha kuvilaani, kwa sababu hamushuguliki hata kidogo na maagizo yangu.


Nani anayeweza kuhesabu wingi wa watu wa Yakobo, au kuhesabu makundi ya Waisraeli? Nikufe kifo cha haki, mwisho wangu ukuwe kama wao.


Heri wale wanaokuwa na huzuni, maana Mungu atawafariji!


Wangekuwa na hekima wangejua kwa nini walishindwa, wangeweza kuelewa mwisho wao utakuwa namna gani.


akawaambia: “Muweke ndani ya mioyo yenu maneno yote ambayo ninawapa leo. Muwaamuru watoto wenu kusudi wafuate kwa uaminifu maneno yote ya sheria hii.


Mwisho wao ni uharibifu, sababu mungu wao ni kushibisha tumbo zao. Wanajivuna kwa kufanya mambo ya kuwafezehesha. Nayo mafikiri yao ni juu ya vitu vya dunia hii.


Kila mutu anapaswa kufa mara moja tu, na nyuma ya kufa, anahukumiwa na Mungu.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan