19 Hekima inamufanya mwenye hekima kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi katika muji.
Mwenye hekima anaweza kuteka muji wa wenye nguvu na kukiporomosha kikingio wanachokitegemea.
Kuwa na hekima na maarifa ni bora kuliko kuwa na nguvu.
Nina uwezo wa kushauri na kuamua vizuri. Nina ufahamu na nina nguvu.
Afazali kijana masikini mwenye hekima kuliko mufalme muzee mupumbafu, ambaye hasikilizi shauri jema,
Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.