Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 7:14 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

14 Katika siku za kufanikiwa ukuwe na furaha. Katika siku za hasara ufikiri juu ya jambo hili: Mungu amefanya hiyo ya kwanza iambatane na ya pili kusudi mwanadamu asipate kujua mambo yatakayotukia nyuma yake.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 7:14
35 Iomraidhean Croise  

kama watakapokuwa kule katika uhamisho wakijifikiri ndani yao wenyewe na kukugeukia, kama katika ile inchi ya uhamisho wakikusihi na kusema ‘Tumetenda zambi; tumepotoka na kufanya maovu’,


Akamujibu: “Wewe unasema kama wanawake wapumbafu. Tukipokea mazuri kutoka kwa Mungu, kwa nini tukatae kupokea vilevile mabaya kutoka kwake?” Katika mambo hayo yote, Yobu hakusema neno lolote la kumukosea Mungu.


Nimefaidika kutokana na taabu yangu, maana imeniwezesha kujifunza masharti yako.


Aliniondoa katika shimo la hatari, alinitoa katika matope mengi, akanisimamisha salama juu ya mulima, na kuziimarisha hatua zangu.


Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.


Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Muhubiri anasema hivi: Bure, bure kabisa. Vyote ni bure.


Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?


wakati wa kulia na wakati wa kucheka, wakati wa kuomboleza na wakati wa kucheza,


Basi, haya ndiyo niliyotambua: jambo zuri na lenye kufaa kwa mwanadamu ni kula, kunywa na kufurahia matunda ya jasho anayotoa hapa chini ya jua, siku zile chache za maisha aliyojaliwa na Mungu, maana hivi ndivyo alivyopangiwa.


Hajui ni kitu gani kitakachotukia nyuma, maana ni nani anayeweza kumujulisha yatakayotukia nyuma?


Kwenda ukule chakula chako kwa furaha, na ukunywe divai yako kwa moyo wenye kuchangamuka, maana Mungu amekwisha kukubali kazi yako.


Ee Yawe umeinua mukono kwa kuwaazibu, lakini hawauoni. Uwaonyeshe namna unavyowapenda watu wako nao watapata haya. Moto unaowatayarishia waadui zako, uwateketeze!


Kwa hiyo aliwamwangia kasirani yake kali, akawaacha kupatwa na vita kali. Hasira yake iliwawakia kila upande, lakini wao hawakuelewa chochote; iliwachoma, lakini hawakufikiri juu ya jambo hilo.


Hasira ya Yawe haitatulia, mpaka atakapotimiza na kukamilisha mapenzi ya moyo wake. Kutakuja siku ambapo mutaelewa vema mambo hayo.


Maovu na mema yanatokea tu kwa amri ya Mungu Mukubwa.


Yawe anawaita wakaaji wa muji, na ni jambo la hekima sana kumutii yeye: Musikilize, enyi watu wa Yuda; musikilize enyi muliokusanyika katika muji.


Muende kujifunza maana ya Maandiko Matakatifu yanayosema: ‘Ninataka huruma, lakini si sadaka zenu.’ Kwa maana sikukuja kuwaita wenye haki kunifuata, lakini watenda mabaya.”


Kule waliwajenga wanafunzi moyo na kuwatia nguvu wabakie katika imani wakiwaambia: “Ni sherti tupite katika mateso mengi kwa kuweza kuingia katika Ufalme wa Mungu.”


Nawe utafurahia mema yote ambayo Yawe, Mungu wako, amekujalia wewe na jamaa yako. Nao watafurahi pamoja nawe.


“Yawe, Mungu wenu aliwabariki katika kila njia, lakini ninyi hamukumutumikia kwa moyo wa furaha na shangwe.


Aliwazarau akawaacha muone njaa na kisha akawapa mana mukule, chakula ambacho hamukukijua, wala babu zenu hawajapata kukijua. Alifanya hivyo kusudi apate kuwafundisha kwamba mwanadamu haishi kwa mukate tu, lakini kwa kila neno Yawe analosema.


Mukumbuke kwamba Yawe, Mungu wenu, anawaazibu kama vile baba anavyoazibu mwana wake.


Kati yenu kuna mutu anayekuwa katika mateso? Aombe kwa Mungu. Au kuna mutu anayekuwa katika furaha? Aimbe nyimbo za sifa.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan