Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 7:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Kulindwa na hekima ni kama kulindwa na feza. Faida ya maarifa ni kwamba hekima inalinda maisha ya mutu anayekuwa nayo.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 7:12
25 Iomraidhean Croise  

Si wewe mwenyewe unamulinda pande zote pamoja na jamaa yake na kila kitu anachokuwa nacho? Wewe umemubariki na mali yake imeongezeka katika inchi.


Kwa mukubwa wa waimbaji. Kwa mutindo wa wimbo “Usiharibu.” Mashairi ya Daudi alipomuponyoka Saulo na kujificha katika pango.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Masikini anachukiwa hata na jirani yake, lakini tajiri ana warafiki wengi.


Hekima itakulinda, ufahamu utakuchunga;


Anawawekea watu wa usawa akiba ya hekima safi, yeye ni ngao kwa watu wanaoishi kwa ukamilifu.


Hekima ni muti wa uzima kwa wote wanaoipata; wana heri wote wanaoshikamana nayo.


Anayenipata mimi amepata uzima, na upendeleo kutoka kwa Yawe.


Kwa musaada wangu mimi Hekima siku zako zitaongezwa; utaongezewa miaka mingi katika maisha yako.


Chakula ni kwa ajili ya kujifurahisha, divai inachangamusha maisha, na feza inasababisha hayo yote.


Basi, mimi nikagundua kwamba hekima ni bora kuliko upumbafu, kama vile mwangaza unavyokuwa bora kuliko giza.


Hekima inamufanya mwenye hekima kuwa na nguvu zaidi kuliko watawala kumi katika muji.


Basi, mimi ninasema, hekima ni bora kuliko nguvu, ingawa hekima ya masikini inazarauliwa, na maneno yake hayasikilizwi.


Kuwa na hekima ni bora kuliko kutegemea silaha, lakini mwenye zambi mumoja anaharibu mazuri mengi.


Bila kutaka shauri langu, wanafunga safari kwenda Misri, kukimbilia ulinzi kwa mufalme wa Misri, kupata pahali pa kujificha katika inchi yake.


Kila mumoja atakuwa kama pahali pa kujikinga na upepo, kama pahali pa kujificha wakati wa mvua kubwa. Watakuwa kama vijito vya maji katika inchi yenye kukauka, kama kivuli cha jiwe kubwa katika jangwa.


Enyi watu wa Yerusalema, Yawe atawajalia usalama, atawaokoa na kuwapa hekima na maarifa. Akiba yenu kubwa ni kumwogopa Yawe.


Nami ninajua kama amri yake inaleta uzima wa milele. Ni kwa hiyo maneno ninayosema, ninayasema tu kama vile Baba alivyoniagiza.”


Nao uzima wa milele ni kukujua wewe unayekuwa peke yako Mungu wa kweli na Yesu Kristo uliyemutuma.


Maana sheria hii si maneno matupu lakini ni uzima wenu; kwa njia ya sheria hii, mutaishi maisha marefu katika inchi munayokwenda kurizi, ngambo ya muto Yordani.”


Bila shaka, ninahesabu mambo yote kuwa kihombo kwa ajili ya faida kubwa ya kujua Kristo Yesu Bwana wangu. Kwa ajili yake nimekubali kupoteza vyote, nikivihesabu kuwa kama mavi, kusudi nimupate Kristo


Muti wa miiba ukajibu: ‘Kama kweli munataka kunichagua kuwa mufalme, mukuje mukae chini ya kivuli changu. Lakini kama hamutaki kufanya hivyo, basi moto utoke kwenye miiba yangu na kuiteketeza hata mierezi ya Lebanoni.’ ”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan