Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 6:7 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

7 Mutu anatoa jasho kwa ajili ya kupata chakula, lakini tamaa yake ya kula haitoshelezwi hata kidogo.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 6:7
11 Iomraidhean Croise  

Njaa inamusukuma mutu kufanya kazi, maana tamaa ya kinywa chake inamupa bidii.


Mambo yote yanasababisha muchoko, muchoko mukubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.


Mali ikiongezeka, wale watakaoikula wanaongezeka vilevile, naye mwenye mali inamufalia nini isipokuwa kuiangalia tu mali yake?


Yule anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayetamani mali hata akiipata hatatosheka. Hayo nayo ni bure.


Mutu akiweza kuzaa watoto mia moja, na akiishi maisha marefu, lakini kama mutu huyo hafurahii maisha yake, wala hafanyiwi mazishi, basi ninasema mutoto aliyezaliwa amekufa ni afazali kuliko mutu yule.


Basi mutu mwenye hekima ana faida zaidi kuliko mupumbafu? Na mutu masikini anapata faida gani akijua namna ya kuishi?


“Ni kwa sababu hii ninawaambia ninyi: musijisumbue kwa ajili ya maisha yenu, kwa ajili ya chakula au kwa ajili ya kinywaji, wala musijisumbue kwa ajili ya miili yenu kwamba mutavaa nini. Uzima ni wa lazima kuliko vyakula, nao mwili ni wa lazima kuliko nguo.


Kisha nitajisemesha hivi juu yangu mwenyewe: ‘Uko na mali nyingi ulizoweka akiba kwa miaka mingi. Sasa utulizane, ukule na kunywa na kujifurahisha.’


Musitumikie chakula kinachoharibika, lakini mutumikie chakula kinachodumu na kuleta uzima wa milele. Mwana wa Mutu atawapa ninyi chakula hiki, kwa sababu Mungu Baba ametoa uhakikisho juu yake.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan