Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 6:12 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

12 Nani anayejua yanayofaa kwa mutu katika maisha haya mafupi yasiyokuwa na faida, maisha ambayo yanapita kama kivuli? Nani anayejua yale yatakayotukia chini ya jua nyuma ya kufa kwake?

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 6:12
28 Iomraidhean Croise  

Sisi tuko wageni mbele yako, na wasafiri kama vile babu zetu walivyokuwa wote. Siku zetu katika dunia ni kama kivuli kinachopita, hapa hakuna tumaini la kukaa.


Anachanua kama maua, kisha ananyauka. Anakimbia kama kivuli na kutoweka.


Watoto wake wakiheshimika, yeye hana habari. Wakizarauliwa, yeye haoni kabisa.


Sisi ni watu wa juzijuzi tu, hatujui kitu; siku zetu katika dunia ni kivuli kinachopita.


kwa sababu ya kasirani na hasira yako, maana umeniokota na kunitupilia mbali.


Ninatoweka kama kivuli cha magaribi; nimepeperushwa kama nzige.


Mwanadamu ni kama pumzi tu; siku zake zinapita kama kivuli.


Wewe, ee Yawe, ndiwe riziki yangu kubwa, majaliwa yangu yako katika mikono yako.


Lakini mimi nitauona uso wako, maana mimi ni mutu wa haki; nitakapoamuka nitajaa furaha kwa sababu unanitokea.


Mutoe sadaka zinazokuwa sawa, na kumutumainia Yawe.


Ametuwezesha kuwashinda watu wa mataifa, ameyaweka mataifa chini ya mamlaka yetu.


Ee Yawe, utajificha hata milele? Mpaka wakati gani hasira yako itawaka kama moto?


Mupumbafu anasema maneno mengi. Mwanadamu hajui yatakayokuwa, wala yale yatakayotukia nyuma yake.


Nyuma ya hayo yote yaliyokwisha kusemwa, kungali hili linalotakiwa: Umwogope Mungu, na ushike amri zake, kwa sababu hayo ndiyo mapaswa ya mwanadamu.


Hakuna kitu kizuri kwa mwanadamu, isipokuwa kula na kunywa na kufurahia matunda ya jasho yake. Hili nalo nimeliona kwamba linatoka kwa Mungu,


Nilitafuta kwa hekima namna ya kujichangamusha mwili kwa divai na kutenda sawa na wapumbafu. Nilitaka kuona kitu gani ni kizuri kwa wanadamu kufanya wanapoishi maisha yao mafupi hapa chini ya mbingu.


Basi, nikatambua kwamba hakuna jambo linalokuwa bora zaidi kwa mwanadamu kufanya kuliko kufurahia kazi yake, kwa sababu amepangiwa hivyo. Nani anayeweza kumujulisha mwanadamu yale yatakayokuwa kisha kufa kwake?


Maneno yanapokuwa mengi, ndivyo yanaendelea kuwa bure. Hayana faida.


Katika maisha yangu ya bure, niliona kila kitu. Mutu wa haki anakufa ingawa ni wa haki, ambapo mutu mwovu anaendelea kuishi maisha marefu ingawa ni mwovu.


Lakini hakuna furaha kwa waovu. Wao watapita kama kivuli, maisha yao hayatakuwa marefu kwa sababu hawamwogopi Mungu.


Hajui ni kitu gani kitakachotukia nyuma, maana ni nani anayeweza kumujulisha yatakayotukia nyuma?


Upendo wao, chuki zao na tamaa zao, vyote vimetoweka pamoja nao, wala hawatashiriki tena katika kitu chochote hapa chini ya jua.


Furahia maisha pamoja na muke wako unayemupenda muda wote wa maisha yako ya bure ambayo Mungu amekujalia hapa chini ya jua, maana hilo ndilo ulilopangiwa katika maisha, katika kutoa jasho yako hapa chini ya jua.


Mungu amekuonyesha yanayokuwa mema, ewe mwanadamu; kitu Yawe anachotaka kwako ni hiki: kutenda mambo ya haki, kupenda kuwa na huruma, na kuishi kwa unyenyekevu mbele ya Mungu wako.


Ninyi hamujui namna gani maisha yenu yatakavyokuwa kesho! Kwa maana ninyi ni kama muvuke unaoonekana kwa wakati kidogo, kisha unatoweka.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan