Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 5:13 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

13 Kwa bahati mbaya, mali hiyo iliharibiwa katika matumizi mabaya. Kwa mwisho, mutu yule hakukuwa na kitu chochote wakati alipokuwa na mwana.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 5:13
29 Iomraidhean Croise  

Basi, Abramu akakomboa mali yote iliyonyanganywa na waadui, na kumukomboa mwipwa wake Loti, mali yake, pamoja na wanawake na watu wengine.


Basi, Loti akawaendea wachumba wa wabinti zake, akawaambia: “Haraka! Mutoke pahali hapa, maana Yawe atauangamiza muji huu.” Lakini wao wakamwona kama mutu mwenye kuchekesha tu.


Lakini muke wa Loti aliyekuwa nyuma ya Loti, akatazama nyuma, akageuka nguzo ya chumvi.


Kwa vile ulafi wake hauna mwisho, hataweza kuokoa kitu chochote cha lazima.


Ndizo njia za wanyanganyi; maisha yao yananyanganywa.


Maana wajinga wanajiua kwa kiburi chao, wapumbafu wanajiangamiza kwa kufanikiwa kwao.


Utajiri haufai kitu siku ya kasirani, lakini haki inaokoa kutoka kifo.


Usijichokeshe na kutafuta utajiri; acha kufikiri juu yake.


Maana utajiri haudumu milele, wala taji haidumu kwa vizazi vyote.


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Kama vile mwanadamu alivyokuja katika dunia akiwa uchi toka katika tumbo la mama yake, ndivyo atakavyorudi uchi kule alikotoka. Hataweza kupeleka hata sehemu ndogo ya mapato ya kazi yake.


Haya yote nimeyaona katika uchunguzi wangu juu ya yote yanayotendeka hapa chini ya jua, ambako mwanadamu anatawala mwenzake na kumutesa.


Siku hiyo, watu watawatupia panya na popo sanamu za feza na zahabu walizojitengenezea kusudi waziabudu.


Feza yao wala zahabu yao havitaweza kuwaokoa katika siku hiyo ya kasirani ya Yawe. Kwa moto wa wivu wake dunia yote itateketezwa. Kwa ukamilifu na kwa namna ya kuogopesha atawafanya wakaaji wote katika dunia watoweke.


“Kulikuwa mutu mumoja tajiri aliyezoea kuvaa nguo zenye kuwa laini sana za bei kali zaidi na aliyeishi katika raha siku zote.


Lakini Zakayo akasimama mbele ya Bwana na kumwambia: “Bwana! Ninawapa masikini nusu ya mali zangu, na kama nimetwaa kitu cha mutu kwa kumudanganya, nitamurudishia mara ine sawa na kitu kile.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan