Muhubiri 5:11 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002
11 Usingizi wa mutumishi ni mutamu, akuwe ameshiba au amekula kidogo tu. Lakini usingizi wa tajiri ni wa wasiwasi siku zote, maana mali yake inamuzuia kupata usingizi.
Ewe kijana, furahia ujana wako, moyo wako ukuwe na raha wakati ungali kijana. Fuata mapenzi ya moyo wako na tamaa ya macho yako. Lakini kumbuka kwamba Mungu atakuhukumu kadiri ya hayo yote.
Mutu anayepata mali isiyokuwa ya usawa ni kama kwale anayelalia mayai ambayo hakutaga. Mali yanamwishia angali kijana, na kwa mwisho anageuka sawa mupumbafu.
Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.