Kila kitu macho yangu yalichokitamani nilikipata. Moyo wangu sikuunyima raha yoyote. Moyo wangu ulifurahia mambo niliyotenda, na hii ilikuwa zawadi ya jasho langu.
Kisha nikafikiri juu ya yote niliyokuwa nimefanya kwa mikono yangu, na jinsi nilivyotoa jasho kwa kuyafanya. Nikatambua kwamba yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo. Hakukukuwa faida yoyote chini ya jua.
Mungu anamujalia mutu anayependezwa naye hekima, akili na furaha; lakini anamupa mwenye zambi kazi ya kuvuna na kulundika, kisha Mungu anavipatia yule anayemupendeza. Hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Mwisho wa mwanadamu na mwisho wa nyama ni mumoja. Jinsi mwanadamu anavyokufa ndivyo nyama anavyokufa. Wote wanapumua namna ileile; mwanadamu si bora kuliko nyama. Yote ni bure.
Hesabu ya watu haikukuwa na mwisho, naye aliwatawala wote. Hata hivyo, wale wanaozaliwa nyuma hawatamufurahia. Hakika hayo nayo ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.
“Hakuna mutu anayeweza kuwatumikia wabwana wawili. Kwa maana atamuchukia mumoja na kumupenda mwingine; au atashikamana na mumoja na kumuzarau mwingine. Hamuwezi kutumikia Mungu na kutumikia mali vilevile.
Kwa maana kupenda feza ni shina la mabaya yote. Kwa ajili ya kuzitamani watu wamoja wanaanguka katika imani yao, na wanajiumiza mioyo wakijiletea huzuni nyingi.