Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 4:9 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

9 Ni afazali kuwa wawili kuliko mutu kuwa peke yake. Kwa sababu wawili watapata matunda ya jasho yao.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 4:9
15 Iomraidhean Croise  

Kisha Yawe Mungu akasema: “Si vizuri huyu mwanaume kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi wa kumufaa.”


Yoabu akamwambia Abisai: “Ikiwa Waaramu wananizidi nguvu, utanisaidia; lakini kama Waamoni wanakuzidi nguvu, nitakuja kukusaidia.


Chuma kinanoa chuma, vilevile mutu anafundishwa na mwenzake.


Na mumoja akianguka, huyo mwenzake atamusimamisha. Lakini ole wake mutu anayekuwa peke yake akianguka! Huyo hatakuwa na mutu wa kumusimamisha!


Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.


Basi, Yawe akamutia moyo mutawala Zerubabeli wa Yuda pamoja na Kuhani Mukubwa Yoshua na watu wote waliokuwa wamerudi kutoka katika uhamisho. Wakaanza kazi hiyo ya kuijenga upya nyumba ya Yawe wa majeshi, Mungu wao,


Siwezi kuwatunza watu wote hawa peke yangu; kwa sababu ni muzigo muzito kwangu!


Aliwaita wanafunzi wake kumi na wawili, akaanza kuwatuma wawili wawili na kuwapatia uwezo wa kufukuza pepo.


Muvunaji anakwisha kupokea mushahara, naye anakusanya mavuno kwa ajili ya uzima wa milele, kusudi mupandaji na muvunaji wafurahi pamoja.


Siku moja walipokuwa wakifanya ibada, wakiwa wamefunga kula chakula, Roho Mutakatifu akasema: “Muwasimike Barnaba na Saulo kwa kazi ile niliyowachagulia.”


Basi, mujiangalie wenyewe, kusudi musipoteze matunda ya kazi yenu, lakini mupokee zawadi kamili.


Yawe akubariki kwa yote uliyoyafanya. Yawe wa Israeli uliyemukimbilia akulinde chini ya mabawa yake, akupe zawadi kamilifu.”


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan