Biblia Todo Logo
Bìoball air-loidhne

- Sanasan -




Muhubiri 4:8 - BIBLIA Maandiko Matakatifu Kwa Watu Wote 2002

8 Nilimwona mutu mumoja anayekuwa peke yake, hana mwana wala ndugu. Hata hivyo, haachi kutoa jasho. Hatosheki hata kidogo na mali yake wala hatulii na kujiuliza: “Ninatoa jasho kwa ajili ya nani na kujizuiza kuwa na raha?” Hayo nayo ni bure. Ni shuguli inayosikitisha.

Faic an caibideil Dèan lethbhreac




Muhubiri 4:8
21 Iomraidhean Croise  

Kisha Yawe Mungu akasema: “Si vizuri huyu mwanaume kuwa peke yake. Nitamufanyia musaidizi wa kumufaa.”


Kumbe umenipimia maisha mafupi sana! Maisha yangu si kitu mbele yako. Hakika, kila mwanadamu ni kama pumzi tu!


Kweli, kila mutu anapita kama kivuli; masumbuko yake yote ni bure tu; anakusanya mali, hajui atakayeipata!


Kuzimu na shimo la kuangamia havishibi hata kidogo, vilevile macho ya watu hayashibi.


Nilifanya bidii kuchunguza na kutafuta kwa hekima kila kitu kinachotukia chini ya mbingu. Hiyo ni taabu kubwa ambayo Mungu amewapa wanadamu.


Mambo yote yanasababisha muchoko, muchoko mukubwa usioelezeka. Jicho halichoki kuona, wala sikio kusikia.


Maana, wakati mwingine, mutu ambaye amefanya kazi kwa kutumia hekima, akili na maarifa yake, anamwachia mutu mwingine afurahie matunda ya kazi ambayo hakuitoshea jasho. Hayo nayo ni bure. Ni jambo baya sana.


Maisha yake yote yamejaa taabu, na jasho yake ni mahangaiko matupu. Hata usiku akili yake haipumziki! Hayo nayo ni bure.


Tena, niliona jambo moja la bure chini ya jua.


Mali ikiongezeka, wale watakaoikula wanaongezeka vilevile, naye mwenye mali inamufalia nini isipokuwa kuiangalia tu mali yake?


Yule anayependa feza hatatosheka na feza, wala anayetamani mali hata akiipata hatatosheka. Hayo nayo ni bure.


Ole kwao wanaoongeza nyumba juu ya nyumba, wanaoongeza mashamba juu ya mashamba yao, mpaka kila sehemu inakuwa mali yao, na hakuna nafasi kwa wengine katika inchi.


Mbona munatumia feza zenu kwa ajili ya kitu kisichokuwa chakula? Kwa nini kutoa jasho lenu kwa kitu kisichoshibisha? Munisikilize mimi kwa uangalifu, nanyi mutakula vinavyokuwa vitamu, na kufurahia vinavyokuwa bora.


“Mukuje kwangu ninyi wote munaosumbuka na kulemewa na mizigo mizito, nami nitawapumzisha.


Lakini Mungu akamwambia: ‘Mupumbafu wewe! Leo leo usiku utakufa. Na sasa, vitu hivi vyote ulivyojitayarishia vitakuwa vya nani?’ ”


Kwa maana kila kitu kinachokuwa katika dunia, kama vile tamaa ya kimwili, tamaa ya macho, na majivuno ya maisha, hivi vyote havitoki kwa Baba, lakini vinatoka katika dunia.


Lean sinn:

Sanasan


Sanasan