3 Lakini heri zaidi kuliko wafu na wanaokuwa wazima, yule ambaye bado hajazaliwa na kuona maovu yote yanayotendeka hapa chini ya jua.
Mutu kama yule atashangilia sana na kufurahi atakapokufa na kuzikwa!
Nimeyaona mambo yote yanayofanywa chini ya jua. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo!
Kwa hiyo, nikachukia maisha, maana yote yanayotendeka chini ya jua yalinisikitisha. Yote ni bure sawa na kutaka kukamata upepo.
Wanawake wenye mimba na wenye kunyonyesha watapata hasara katika siku zile!
Kwa maana siku zitakuja wakati watu watakaposema: ‘Heri wanawake wanaokuwa tasa, wale waliokosa kuzaa na kunyonyesha!’